The House of Favourite Newspapers

20 Percent: Kila niliyetoka naye ana mwanangu

0

Msanii Abbas Kinzasa a.k.a 20%Na Gabriel Ng’osha

BAADA ya kumaliza tofauti zake na mtayarishaji wa muziki, Man Walter, Msanii Abbas Kinzasa ’20 Percent’ anayetarajia kutoa wimbo mpya wa Sitoi amefunguka kuwa wanawake wote alio-date nao kila mmoja ana damu yake.

Akifungukia historia ya maisha yake ya kimapenzi 20 Percent alisema kuwa, kila msichana aliyempitia aliishia kuzaa naye na sasa ana watoto zaidi ya wawili na kila mmoja na mama yake.

“Ni suala la maamuzi tu kaka ila kiukweli watoto ninao zaidi ya wawili, kwani sehemu kubwa ya wanawake niliotoka nao kimapenzi wana damu yangu,’’ alisema 20 Percent.

Leave A Reply