The House of Favourite Newspapers

Vodacom na Samsung Zawaletea Galax S7 Na S7 Edge Zisizoingiza Maji‏

0

????????????????????????????????????

Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(wapili kushoto)akionesha simu ya kisasa aina ya Galax S7 kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa uzinduzi wa simu hizo aina ya Galax S7 na S7 Edge ambazo haziingizi maji ulifanyika Makao Makuu ya Kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na Samsung Tanzania, Kutoka kushoto Meneja wa bidhaa wa Samsung,Rayton Kwembe, Mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa wa Vodacom Tanzania, Samson Charles na Meneja masoko wa Samsung,Tulisindo Mwachula.

????????????????????????????????????

Meneja wa bidhaa wa Samsung,Rayton Kwembe(kushoto)akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi unavyoweza kuitumia simu ya aina ya Galax S7 na S7 Edge katika matumizi mengine, wakati wa uzinduzi wa simu hizo ambazo haziingizi maji ulifanyika Makao Makuu ya Vodacom Tanzania Mlimani City jijini Dar es Salaam, Katikati Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu na Mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa wa Vodacom Tanzania, Samson Charles.

????????????????????????????????????

Meneja wa bidhaa wa Samsung, Rayton Kwembe (kushoto) Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu, Mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa wa Vodacom Tanzania,Samson Charles, Meneja masoko wa Samsung, Tulisindo Mwachula, wakionesha simu aina ya Galax S7 na S7 Edge kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa simu hizo ambazo haziingizi maji ulifanyika Makao Makuu ya Vodacom Tanzania Mlimani City jijini Dar es Salaam.

????????????????????????????????????

Meneja wa bidhaa wa Samsung,Rayton Kwembe(kushoto) na Mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa wa Vodacom Tanzania, Samson Charles (kulia) wakimshuhudia Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu, akiwaonesha waandishi wa habari(hawapo pichani)simu ya kisasa aina ya Galax S7 wakati wa uzinduzi wa simu za aina hiyo na S7 Edge ambazo haziingizi maji ulifanyika Makao Makuu ya Kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na Samsung Tanzania.

Tukiwa kampuni inayoongoza  kwa mawasiliano hapa nchini leo tunautangazia Umma kwa kuzindua mauzo ya simu za kisasa kabisa ulimwenguni na ambazo haziingizi maji, Galax S7 na S7 Edge kwa kushirikiana na kampuni ya Samsung.
Simu hizi mbili ambazo tumezizindua leo na kuanzia sasa zitakuwa zinapatikana katika maduka yote ya Vodacom pamoja na ya Samsung kote nchini.Tukiunga mkono jitihada zinazofanywa na Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA)kwa wananchi kutokuuziwa simu zisizokidhi kiwango cha ubora wa simu yaani(Simu feki).
“Samsung Galaxy S7 na Galaxy S7 Edge zitakuwa zikitolewa kupitia maduka yetu yote huku zikiambatanishwa na Power-Bank ya BURE; ambapo vilevile, kwa wanunuaji 50 wa kwanza wataweza kujipatia Bluetooth Earphones za Galaxy za bure kabisa,” Alisema Matina Nkurlu, Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania.
Nkurlu alibainisha kwamba,Simu hizi mbili zimekuja zikiwa na maboresho mahsusi yanayolenga kukidhi mahitaji ya vijana wa kisasa hususani katika msimu huu wa sikukuu ya Pasaka, ambapo watumiaji wataweza kufurahia na internet ya kasi na haraka zaidi kupitia mtandao wa Vodacom.
Leave A Reply