The House of Favourite Newspapers

Amber Lulu abanwa skendo ya ukuwadia mamodo

0

amber luluNa Hamida Hassan

VIDEO Queen aliye ‘hot’ Bongo, Lulu Auggen ‘Amber Lulu’ anadaiwa kuwakuwadia mastaa wenzake kwa mapedeshee kiasi cha kuwa maarufu kwa jina la wakala wa Ma-video Queen ‘mamodo’.

Mmoja wa warembo aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini alisema kuwa, mwanadada huyo amekuwa akifanya mchezo huo kwa muda mrefu kiasi cha kujiingizia kipato kikubwa.

“Yule namjua vizuri, aliwahi kuniunganisha na jamaa mmoja ambaye nilimkubalia kutokana na njaa zangu, hee! Siku nyingine si akanipigia tena kuniambia eti kuna mtu ananihitaji, nikajua ni kuwadi,” alisema mtoa habari huyo.

Katika kupata ukweli wa madai hayo, paparazi wetu alimtafuta Amber Lulu,  alipopatikana na kubanwa alisema: “Ni kweli wapo watu wananipaga dili za kuwaunganisha na mastaa, sasa nitaachaje hela wakati maisha yenyewe ndiyo haya.”

Leave A Reply