Barcelona yavunja Mkataba na Guardiola
Sergi Guardiola.
Barcelona, Hispania
KLABU ya Barcelona nchini Hispania imeingia kwenye headline leo baada ya kuvunja mkataba wake na mchezaji Sergi Guardiola saa moja tu baada ya kumsajili.
Hii imetokea baada ya Sergi Guardiola (hana uhusiano na kocha Pep Guardiola) kuandika kwenye mtandao wa twitter maneno ambayo yanaonesha kuuchukiza uongozi wa Barca.
Maneno aliyoandika Sergi mtandaoni: dating back to 2013
Kiungo Guardiola mwenye umri wa miaka 24, kabla ya kujiunga na Barca alikuwa akichezea timu ya Alcorcon inayoshiriki ligi ndogo za Hispania.
Walichokisema Barca kuhusu Guardiola ni hiki hapa.
FC Barcelona imeamua kuvunja mkataba wake iliosaini na Sergi Guardiola ambaye pia aliingizwa kwenye kikosi B cha Barcelona, baada kugundua kuwa ameandika kwenye mtandao wa twitter maneno yanayolenga kuichafua klabu ya Barca and Catalonia.
Sergi alipohojiwa na kituo cha redio cha Cope nchini humo alisema: “Nafahamu nimetanda kosa. Naomba msamaha kwa Catalonia and Barcelona. Nafahamu maamuzi yaliyofikiwa dhidi yangu”.
“Nataka niweke wazi kwamba. Hayo maneno yaliyozagaa kwenye twitter sikuandika mimi, bali ni rafiki yangu ndiye aliyechukua suimu yangu na kufanya hivyo. Tumeshindwa kuelewana. Tweet ni ya kuanzia mwaka 2013, ni matani tu ya rafiki yangu, sikufahamu kabisa kama kuna tweet ameiweka mtandaoni inayonihusu mimi.
Sergi Guardiola Best Skills & Highlights FC Barcelona 2015/2016 pic.twitter.com/vAgOXEZmr4
— Eles (@Elestinho) December 28, 2015
Sergi Guardiola. Signs for Barcelona B. One hour later, club release him after checking those tweets. Legend. pic.twitter.com/EAM2tTbH8W
— Ali (@RM_Insider) December 28, 2015
[FOTOS] Les noves incorporacions, a punt per començar a entrenar https://t.co/qw4PIIqIse #FCBB #FCBMasia #2bg3 pic.twitter.com/ardWoVb7cw
— FC Barcelona – Masia (@FCBmasia) December 28, 2015