The House of Favourite Newspapers

Chezea waosha magari wewe!

3

Sasa jamani mbona hivyo tena? Mi sio mhariri wa hili gazeti sasa mbona mnaniletea maswali magumu? Yaani kuna mdada kanitumia barua juzi anataka ushauri nimebaki nimeduwaa sina la kusema kabisa. Ninachoweza kusema ni kuwa sasa nina uhakika wa ule msemo wa wahenga kuwa Kupenda Upofu. Hebu na nyinyi someni wenyewe mi nakaa pembeni!
Anko Shikamoo,

Vipi mzima? Anko mie huwa napenda sana kusoma makala zako, zinanifurahisha sana, nikisoma naona kuwa wewe una busara sana sasa nimepata tatizo naomba unipe ushauri babu yangu. Naomba unisaidie pliz.
Anko huu ni mwezi wa nne tangu nimeolewa, yaani tayari najilaumu sana kuhusu ndoa hii. Kiukweli najuta sana. Kabla ya kunioa mume wangu alikuwa anakuja kwangu kila siku na gari jingine, akaniambia kazi yake ni dalali wa magari na akaniahidi kuwa na mimi ataninunulia gari ili nisiwe na tatizo la usafiri.
Niliongeza mapenzi kwake ili asijekusahau kunipa gari. Uchumba wetu ulichukua miezi mitatu kisha tukaoana katika ndoa ambayo mpenzi wangu alisema tufanye kakitu kadogo tu kakisiri tusiharibu pesa. Ndugu zangu walininunia lakini mimi sikujali.

Kwa kuwa nilikuwa na chumba kizuri katikati ya mji, ilionekana maisha tuanze kwetu maana mume wangu alisema alikuwa akiishi na mama yake nje ya mji, aliyekuwa akimkataza asipange chumba. Huwezi kuamini Anko, si juzijuzi tu ndiyo nimegundua kumbe nilikuwa nadanganywa siku zote, kumbe mume wangu kazi yake ni kuosha magari, hana udalali wala nini.

Kuna kijiwe chao kando ya mto wanaosha magari mchana kutwa sasa akiachiwa aoshe gari basi ndiyo huzunguka nalo na ndipo alipoweza kunidanganya nikaingia kingi. Kwa nini alinidanganya vile? Si angenieleza tu ukweli nijue? Ntaendeleaje kumuamini sasa?  Mbaya zaidi mi nimemaliza chuo kikuu na  nimegundua kuwa jamaa hakumaliza hata fom tu,  Anko what do I do?

Wenzangu walikuwa wananicheka nilikuwa siwaelewi. Nilikuwa kila siku napiga picha niko kwenye gari tofauti nazituma Instagram, jamani watu wakigundua si ndiyo watanichamba mwaka mzima? Ndugu zangu walinionya kuwa wanamuona jamaa tapeli nikagombana nao sana, narudije kwetu? Anko nipe ushauri.
Hata mimi sijui nimwambieje huyu mdada, hivi alikuwa mjinga kiasi gani hakuona kuwa anatapeliwa?

3 Comments
  1. JOJO says

    Jamani kama huyo jamaa nimuosha gari kwani ubaya uko wapi kwani siyo kazi au hana pesa za kukutunza? Kama kweli unampenda nayeye anakupenda naona hamna tatizo umeshaolewa basi ishi nae ila mshauri aongeze elimu.

  2. Mapuma miyoga says

    Jamaa yuko vema. Akina dada si ndio mnataka hivyo, uongo uongo ndio huwapa furaha na kuamua kufunua Self za BOT zenu.

  3. mjumbe says

    kama alikuwa anamlidhika hakuna tatizo. wamependana.

Leave A Reply