Chozi la Kanumba kwa Maya halikauki
Mayasa Mrisho ‘Maya’ na Kanumba enzi za uhai wake.
STORI: Imelda Mtema, Wikienda
Dar es Salaam: Mwigizaji wa kitambo Bongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amefunguka kuwa chozi lake kwa aliyekuwa mwigizaji mwenzake aliyemfanya kaka yake wa hiari, marehemu Steven Kanumba halikauka siku zote pamoja na kwamba ni takriban miaka minne tangu alipoaga dunia Aprili 7, 2012.
Maya akiliakwa uchungu
Akizungumza na Wikienda, Maya alisema kuwa, mara nyingi watu huwa hawamuelewi lakini ukweli ni kwamba thamani ya uigizaji wake imepotea tangu alipoondoka Kanumba kwani ndiye aliyekuwa akimtia moyo.
Marehemu Kanumba
“Tunaweza kuwa lokesheni, nikajikuta nikidondosha machozi na hapo watu watafanya kazi sana kuniweka sawa ili niweze kuendelea. Ni kama maisha yangu kwani mara nyingi najikuta nalia sana kwa ajili ya Kanumba,” alisema Maya aliyekuwa mtu wa karibu wa staa huyo.