The House of Favourite Newspapers

Denti uhasibu akatwa miguu

0

Beatrice Ndomba baada ya kukatwa miguu yake yote miwili na       kuwa mwenye ulemavu wa viungoBeatrice Ndomba akiwa amekatwa miguu.

Na Stephano Mango, UWAZI

RUVUMA: Beatrice Ndomba (23) amelazimika kukatisha masomo kwenye Chuo cha Uhasibu jijini Mbeya mwaka 2012 baada ya kuugua ugonjwa uliogharimu miguu yake.

Msichana huyo anasema kuwa, mwaka 2012 akiwa chuoni hapo, alianza kujisikia hali ya homa, ikabidi arudi kwao, Songea mkoani Ruvuma kwa matibabu.

Alisema tatizo lilianza mwaka 2012 akiwa amejiunga na masomo ya stashada ya uhasibu kwenye Chuo cha Uhasibu jijini Mbeya ambapo alianza kupata maumivu makali kwenye mguu mmoja hali iliyomsababishia kushindwa kuendelea na masomo.

“Ilianza dalili ya homa kama malaria,  nilipewa dawa za SP ambazo hazikunisaidia, ndipo nilipelekwa Hospitali ya Songea ambako nilitundikiwa dripu ya kwinini, pia haikusaidia, sasa ikawa maumivu makali  kwenye miguu yote.

Beatrice Ndomba kabla hajapata ulemavu wa kukatwa miguu        yote miwiliKabla ya kukatwa miguu

“Ilibidi nipelekwe Hospitali ya Rufaa ya Misheni Peramiho ambapo madaktari walijitahidi lakini wapi. Miguu  ikaanza kuvimba na kuwa na rangi nyeusi, madaktari walishauriana na kuamua kuichubua ngozi na kutibu vidonda.

“Uchunguzi zaidi ulifanywa na ulibaini kuwa, mguu mmoja uliharibika hivyo waliamua kuukatia jirani ya goti, ndipo ulemavu ukaanzia hapo.

“Madaktari waliniambia chanzo cha tatizo ni matumizi ya  dawa za SP na dripu la kwinini. Kidonda kiliendelea kunisumbua kuanzia mwaka 2012 hadi 2014 na kunisababishia gharama kubwa ya nauli na matibabu ya kwenda Peramiho kila baada ya siku moja.

“Wataalam wa viungo kwa walemavu wa Wilaya ya Mbinga (Ruvuma) walitaka kunitengenezea mguu wa bandia,  lakini nilipochunguzwa kwa makini walibaini kunitengenezea mguu wa bandia isingesaidia kwa kuwa mguu mwingine nao ulikuwa na matatizo makubwa ambayo yalitakiwa kwanza kufanyiwa uchunguzi katika hospitali nyingine.

“Julai 2014, Sista Lucy wa mjini Songea alinisaidia nauli na fedha za matibabu na matumizi kwenda Hospitali ya Misheni ya Ikonda wilayani Makete mkoani Njombe ambayo inatajwa kuwa na madaktari bingwa wa matatizo ya viungo vya binadamu ambako nilikatwa mguu wa pili.

“Kwa sasa ndoto zangu za kuwa mhasibu zimeyeyuka kwa kwa ulemavu huu, siwezi tena kuwa mhasibu badala yake sasa napenda kujifunza zaidi lugha ya Kiingereza, kusomea kompyuta na kujifunza ufundi wa kushona nguo na kudalizi vitambaa.

“Ndoto zangu sasa ni kufungua kiwanda cha ushonaji kwa kuanzia nikipata mashine mbili nitaweza kujitegemea. Nawaomba Watanzania wanisaidie mashine na misaada mingine, nitashukuru sana,” alisema.

Beatrice ambaye ni yatima, ndiye mtoto wa kwanza  katika familia ya watoto tisa,  anahitaji msaada wa hali na mali katika kipindi hiki ambacho hana ajira zaidi ya kutegemea misaada ya wahisani.

Hata hivyo, yeye na wadogo zake  wamefadhiliwa kuishi kwenye nyumba moja iliyopo Ruhuwiko Manispaa ya Songea.

Kwa wenye kuguswa na habari ya Beatrice wanaweza kumsaidia kupitia namba; 0766 642634 au 0673 054535.

KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP

*********

JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU

KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA

INSTAGRAM: @Globalpublishers

ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo

TWITTER: @GlobalHabari

FACEBOOK: @GlobalPublishers

SUBSCRIBE YOU TUBE: Global TV Online

GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com

HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE:@shigongotz

Leave A Reply