The House of Favourite Newspapers

‘Door of No Return’: Mlango Uliopitisha Mamilioni ya Waafrika Kwenda Utumwani

door-of-no-return gor1

‘Door of No Return’.

gor3

Rais Barack Obama na mkewe wakiwa ‘Door of No Return’  walipotembelea kisiwa cha Gorée Juni 27, 2013.

President Barack Obama looks out of the "door of no return" during a tour of Goree Island, Thursday, June 27, 2013, in Goree Island, Senegal. Goree Island is the site of the former slave house and embarkation point built by the Dutch in 1776, from which slaves were brought to the Americas. The "door of no return" was the entrance to the slave ships. (AP Photo/Evan Vucci)

Obama akiangalia mandhari ya eneo hilo.

MTU  anayepata fursa ya kufika nchini Senegal, Afrika Magharibi,  ni vyema pia akakitembelea kisiwa cha Gorée kilichopo kilomita tatu kutoka pwani ya Jiji la Dakar ambapo, miongoni mwa mambo mengine, ataona  kile kiitwacho kwa Kiingereza ‘Door of No Return’ yaani mlango ambao ukishaupita hutaweza kurejea tena.

Mlango huo upo katika jengo kubwa la zamani lijulikanano kama ‘House of Slaves’ au Jumba la Watumwa.  Kwa Kifaransa linaitwa ‘Maison des Esclaves’.  Mlango huo ulikuwa ndiyo mapito ya mwisho ya Waafrika waliokuwa wanasombwa kwa mamilioni kwenda utumwani sehemu mbalimbali duniani, hususani Bara la Amerika. 

Kwa mtumwa ukiupita mlango huo basi unaelekea moja kwa moja kwenye majahazi au meli zilizokuwa zimetia nanga na kuanza safari ya maelfu ya maili kwenda utumwani ambako walilowea  kwenda kufanyishwa kazi kwa nguvu, wakafia huo na kuacha vizazi ambavyo hadi leo vipo Marekani, Uingereza, Cuba na kadhalika.

Jengo hilo lililokarabatiwa kidogo, lilijengwa mnamo 1776 na kuendelea kuweka namba kubwa ya watumwa hadi mwanzoni mwa miaka ya 1800, pamoja na takwimu zinazokinzana hasa kutoka kwa Wazungu, mlango wake unaaminika ulipitisha Waafrika zaidi ya milioni 15 kwenda utumwani hususan Amerika.

Jumba hilo pamoja na kuwa kivutio cha kusikitisha kwa Waafrika, limetembelewa na watu kibao duniani wakiwemo Papa John Paul wa Pili, Rais Barack Obama, na marehemu Nelson Mandela ambaye kufika kwake hapo kulimtoa machozi hadharani.

Na Walusanga Ndaki

Comments are closed.