RAPA Aubrey Drake Graham, ‘Drake’ amempa hadhi ya juu mwanadada Taylor Swift ikiwemo kumtambulisha kwa mama yake pamoja na watu wake wa karibu zikiwa ni ishara za awali za kuonyesha mahusiano yao.
Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita wakati wa sherehe ya Drake kutimiza umri wa miaka 30 iliyofanyika Los Angeles nchini Marekani.
Drake na Taylor mwaka 2013.
Kitendo hicho kimemake headlines katika mitandao ya kijamii kikiashiria Drake na Taylor kuwa na mahusiano huku kikiongezwa uzito na mwanadada Rihanna ambaye hakuhudhuria sherehe hizo.
Drake na Rihanna.
Kwa mujibu wa chanzo kilichokaribu na Rihanna ambaye ndiye mpenzi wa Drake, ni kwamba alihuzunika baada ya Taylor kuonekana kuchukua nafasi yake kwa kuwa gumzo katika sherehe hiyo na kuwa staa huyo anajilaumu kwa nini hakuudhuria sherehe.
Rihanna na Taylor mwaka 2009.
Comments are closed.