The House of Favourite Newspapers

Duh! Eti Kiiza, Ngoma watachemsha tu

0

Donald Ngoma
KAMA akitamka maneno haya mbele ya mashabiki wa Simba na Yanga, basi anaweza kuingia katika wakati mgumu.

Ofisa Habari wa Ruvu Shooting ya Daraja la Kwanza, Masau Bwire amesema mastraika Hamis Kiiza wa Simba na Donald Ngoma wa Yanga hawatafanya lolote katika mchezo wa leo.

Wakati leo Jumamosi Ruvu Shooting ikicheza mechi ya daraja la kwanza dhidi ya Njombe Mji mjini Njombe, Simba na Yanga zenyewe zinapambana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika Ligi Kuu Bara.

Bwire aliliambia Championi Jumamosi kuwa, mara zote mechi za Simba na Yanga hukosa ufundi hivyo ni ngumu kwa mchezaji nyota kuonyesha uwezo wake halisi, hivyo Ngoma na Kiiza wataonekana wa kawaida tu.

Kiiza ndiye nyota wa Simba kwa sasa akiongoza kwa ufungaji kwa mabao matano aliyonayo wakati Ngoma naye anag’ara Yanga akiwa amefunga mabao matatu sawa na Amissi Tambwe kikosini.

“Siku zote mechi hii ya watani huwa ya kukamiana na kupoteza hata ladha ya mchezo, kama kuna mtu anadhani Kiiza au Ngoma mmoja wao atafanya vizuri huyo atakuwa anakosea.

“Ngoma na Kiiza wanaonekana wazuri, ushishangae wakapoteana kabisa kutokana na soka la hovyo litakalochezwa na timu hizi,” alisema Bwire.

 

 

 

 

 

 

Leave A Reply