Eddy Kenzo Aanika Figisu Alizofanyiwa Kwenye Tuzo za MTV
MKALI wa muziki kutokea nchini Uganda, Eddy Kenzo wa Uganda, amweka wazi sababu za yeye kushindwa kufurukuta kwenye tuzo ya MTV MAMA 2016 zilizofanyika kwenye Ukumbi wa Ticketpro Dome, Johannesburg nchini Afrika Kusini, juzi Jumamosi usiku huku akidai kuwa alifanyiwa figisu kuhusu ushindi wake kwenye tuzo hizo.
Eddy Kenzo aliyekuwa ametajwa kwenye kipengele cha Best Live Act amewanga waandaaju wa tuzo huzo kupitia Instagram akidai kuwa waandaji hawakuzingatia kura zilizopigwa.
Amedai kuwa pengine kwakuwa yeye ni balozi wa mtandao wa Airtel huku mdhamini mkuu wa MTV MAMA ni MTN, wameamua kumpa Cassper Nyovest ambaye ni balozi wa mtandao huo nchini Afrika Kusini.
Kenzo anaamini kuwa amefanya makubwa kuliko Nyovest kwa kuwa na show nyingi duniani lakini pia alipata kura nyingi zaidi kwenye kipengele hicho.
Alichokianika Eddy Kenzo:
Mbali na kudai kufanyiwa figusu kwenye tuzo za MTV MAMA 2016, kwa upande wa pili wa shilingi, Kenzo amefanikiwa kutwaa tuzo ya #AEAUSA kipengele cha Best Video of The Year 2016 zilizotolewa nchunu marekani usiku huo wa juzi.
Comments are closed.