EPL: Man City Akiwa Nyumbani Amepigwa 3-1 na Chelsea
KATIKA Mechi ya EPL iliyopigwa leo katika Uwanja wa Etihad nchini Uingereza, Manchester City amepigwa bao 3-1 dhidi ya klabu ya Chelsea.
Huu ni ushindi wa nane mfurulizo kwa klabu ya Chelsea ambayo kwa sasa imeanza kuthibitisha kuwa huenda ikawa bingwa wa ligi hiyo licha ya ugumu uliopo kwenye ligi hiyo kwa msimu huu. Sasa iko kileleni kwa pointi 34 mbele ya Liverpool wenye pointi 30.
Man City walionekana kuelemewa zaidi hasa kipindi cha pili huku wachezaj wake, Fernandinho na Sergio Aguero wote wawili wakipigwa kadi nyekundu na mwamuzi baada ya kufanya makosa uwanjani.
Magoli ya Chelsea yalifungwa na Diego Costa dakika ya 60, Willian dakika ya 70 na Eden Hazard dakika ya 90 huku goli la Man City likipatikana kwa Chelsea kujifunga dakika ya 45 kupitia kwa Gary Cahill.
Chelsea walisafiri katika dimba la Etihad wakiwa na kumbukumbu ya kumfunga Man City katika mechi za Ligi Kuu England mara ya mwisho February 3 2014, leo December 2 2016 Chelsea iliyochini ya kocha Antonio Conte wamefanikiwa kuifunga Man City goli 3-1. Hhuku mara ya mwisho Chelsea kumfunga Man City EPL alimfunga goli 1-0.
Comments are closed.