The House of Favourite Newspapers

Glory Gideon Atwaa Taji la Miss IFM 2016

0

1Miss IFM 2016 Groly Gideon (katikati), akiwa kwenye pozi na mshindi namba mbili Nasra Muna (kushoto), huku kulia akiwa amepozi Neema Michael ambaye alijinyakulia taji namba tatu.

2Miss IFM 2016 Glory Gideon (katikati), akiwa kwenye pozi na washindi wenzake wa pili hadi wa tano muda mfupi baada ya kutawazwa kushikilia taji hilo ndani ya Ukumbi wa King Solomon Namanga jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

3Mshindi namba mbili wa mashindano hayo Nasra Muna (katikati), akicheza staili ya shock ikiwa ni ishara ya kushngilia ushindi huo.

4Wasanii wanaounda kundi la Navy Kenzo wakitumbuiza kwenye mashindano hayo.

5Mamiss wote waliyoshiriki mashindano hayo wakiwa kwenye pozi la pamoja kabla ya majaji kutaja washindi watano wa kinyang’anyiro hicho.

6Majaji wa shindano hilo wakiongozwa na Martin Kadinda wa kwanza kushoto wakijadiliana namna ya kumpata mshindi wa taji hilo.

7Mgeni rasmi wa mashindano hayo ambaye ni Mwenyekiti wa Vyuo Vikuu Tanzania, Zainabu Abdalah Issa akiongea jambo kabla ya mashindano hayo kumalidhika.

8Miss IFM 2015 Sophia Macha akiwa kwenye kiti tayari kwa kuaga na kumkabidhi taji hilo mshindi wa mwaka huu ambaye ni Glory Gideon.

9Mabosi wa mashindano hayo wakiongozwa na Hashim Lundenga wa pili kutoka kushoto wakifuatilia kwa makini mchakato huo.

10Martin Kadinda akimtunza mmoja wa wanenguaji wa kundi la Navy Kenzo wakati akitumbuiza jukwaani hapo.

11Baadhi ya mashabiki wakifuatilia kwa makini mashindano hayo.

USIKU wa kuamkia leo warembo zaidi ya 17 kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) cha jijini Dar, walipanda kwenye jukwaa moja kwa lengo la kumsaka mrembo mmoja atakaye vaa taji la Miss IFM 2016 akimrithi Sophia Macha aliyekuwa akilishikiria taji hilo kwa mwaka uliyopita wa 2015.

Katika harakati hizo Glory Gideon  ndiye aliyeibuka kidedea kwa kutwaa taji hilo akifuatiwa na Nasra Muna aliyetwaa taji namba mbili huku Neema Michael akikamilisha nafasi ya taji la mshindi wa tatu.

Tano Bora ya mashindano hayo ilitangazwa na majaji wote ambapo Jackline Evenest akianza kutajwa na kufuatiwa na Glory Gideon, Nasra Muna ambaye alitajwa sambamba na Neema Michael huku Happiness Mkabiba akifunga pazia la washindi watano bora kwenye kinyang’anyiro hicho kilichofanyika ndani ya Ukumbi wa King Solomoni uliyopo Namanga jijini Dar es Salaam usiku wa kumkia leo.

Habari/Picha: Musa Mateja/GPL

Leave A Reply