The House of Favourite Newspapers

JB: Bora uigizaji kuliko ubunge

1

JB (2)Erick Evarist

MKURUGENZI wa Jerusalem Film Company, Jacob Stephen ‘JB’ ameweka wazi kuwa kamwe hafikirii kuwa mwanasiasa kwani sanaa inamlipa zaidi.

Akizungumza na mwanahabari wetu katika mahojiano mafupi, JB alisema kipindi cha nyuma ziliibuka tetesi kuwa huenda anaweza kuwa mwanasiasa lakini ukweli kutoka moyoni, sanaa inamlipa.

“Sanaa inanilipa, sifikirii kama ubunge au siasa kwa ujumla inaweza kunilipa kama sanaa ambayo naipenda kutoka moyoni. Labda nikupe mfano, kupitia kampuni yangu, nikizalisha filamu moja inatoa ajira kwa wafanyakazi wasiopungua 30, itatoa ajira katika maduka, machinga na sehemu mbalimbali zinazouzwa filamu.

“Sanaa imetoa ajira kwa wasanii Mil 10. Unafikiri hao watu wangefanya nini kama si sanaa?,” alisema JB.

JB aliongeza kuwa, kwa sasa anamuunga mkono mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli kwani mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete ameweka misingi mizuri katika sanaa.

“Kikwete ametusaidia kwa kiasi kikubwa kuitangaza sanaa yetu, amekuwa akishiriki katika shughuli zetu kitu ambacho kwetu sisi kina maana kubwa sana katika suala zima la kututangaza na ndiyo maana tunaunga mkono CCM na ukizingatia Ilani ya CCM ya uchaguzi huu, imetugusa moja kwa moja,” alimalizia JB.

 

1 Comment
  1. […] Chanzo: GPL […]

Leave A Reply