Jenerali Ulimwengu Apata Ajali, Akimbizwa Moi
TAARIFA zilizoufikia mtandao huu zinaeleza kuwa, Mwandishi Mkongwe nchini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Gazeti la Raia Mwema, Jenerali Ulimwengu amepata ajali leo na kupelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili Kitengo cha Mifupa Moi kwa matibabu. Ajali hiyo imehusisha gari alilokuwa akiendesha yeye aina ya Benz na gari nyingine iliyoigonga gari hiyo upande wa ubavuni.