The House of Favourite Newspapers

Kenya: Wanaharakati Waandamana Kwenye Jengo la Bunge Kutaka Kutambuliwa kwa Watu wa Jinsia 3

kenya1NAIROBI, KENYA: Wanaharakati nchini Kenya wameandamana katika majengo ya Bunge kushinikiza kutambuliwa kwa jinsia ya tatu, watu ambao si wa kike au kiume.

Jana ni siku ya kimataifa ya kuhamasisha kuhusu watu kama hao.

Waandamanaji hao wanaungwa mkono na Mbunge Mwaura Isaac, ambaye ameapa kuwatetea watu hao wanaotaka kutambulika kwa watu wa jinsia ya 3.

kenya-2Mbunge Mwaura Isaac ameitaka Serikali kupeleka mabadiliko ya sheria Bungeni ili watu wenye jinsia ya 3 waweze kutambulika rasmi na sheria za nchi.

Mbunge huyo amesema kuwa sheria zilizopo zinawanyanyapaa watu wa jinsia ya 3.

Comments are closed.