Kiba, Diamond, Zari, Wema, Idriss, Wolper na Vee Money Watajwa Kuwania Tuzo Uganda
KAMPALA: Waandaji wa tuzo za mitindo za Abryanz Style and Fashion, wametoa orodha ya wasanii watakaowania tuzo hizo kwa mwaka 2016.
Tuzo ambazo zitatolewa siku ya Ijumaa, Desemba 9 kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Serena iliyopo mjini Kampala.
Katika tuzo hizo, nchi ya Tanzania inawakilishwa na mastaa kadhaa wakiwemo Alikiba, Wema Sepetu, Diamond Platnumz, Martin Kadinda, Sheria Ngowi, Jokate, Jacqueline Wolper, Ommy Dimpoz, Idris Sultan, Jux, Nedy Music na wengine.
Hii ni orodha kamili ya vipengele watakavyowania wasanii wa Tanzania kwenye tuzo hizo.
Comments are closed.