The House of Favourite Newspapers

Kim Kardashian Aifuta Kesi ya Wizi

kim-2Nyota wa uigizaji katika televisheni Marekani Kim Kardashian West ameondoa mahakamani keshi dhidi ya tovuti ya habari za udaku ya MediaTakeOut.

Alikuwa ameishtaki tovuti hiyo kwa kudai kwamba aliigiza kisha ambapo aliporwa vito hotelini Paris.

Lakini sasa mawakili wake wanasema wameafikiana na tovuti hiyo kutatua mzozo huo nje ya mahakama.

kim-1Tovuti hiyo ya MediaTakeOut pia imechapisha taarifa ya kuomba msamaha.

Kando na kudai kwamba Kim Kardashian alikuwa ameigiza wizi huo, tovuti hiyo pia ilidai kwamba alikuwa amewasilisha ombi la ulaghai la malipo ya bima kuhusiana na vito vyake vya mamilioni ya dola vilivyoibwa.

Polisi mjini Paris walisema watu wawili wenye silaha, waliokuwa wamevalia mavazi ya polisi, waliiba sanduku lililokuwa na vito vya Kim Kardashian West vya thamani ya hadi dola milioni 6.7.

Mumewe Kardashian West, Kanye West, ambaye alikuwa akitumbuiza New York wakati wa kutekelezwa kwa vizi huo, alikatiza utumbuizaji wake.

Baadhi wamesema huenda nyota huyo wa uigizaji alijichongea mwenyewe kwa kufichua eneo alimokuwa akiishi na hata kupakia mtandaoni picha za vito alivyokuwa navyo siku chache kabla ya kuvamiwa na wezi ao.

Tangu wakati huo, amekuwa kimya sana mitandao ya kijamii.

Comments are closed.