The House of Favourite Newspapers

Kukopi Sawa Ila Diamond Hii Sasa Ni Too Much

0

Diamond Snaps (174)

Hans Mloli, Dar

TATIZO halipo kwenye ngoma ya Kidogo ya Diamond Platnumz aliyowashirikisha P Square kutoka Nigeria, lakini ishu hapa ni video ya wimbo huo ambayo ni kali lakini imeshuka vyeo kutokana na ‘copy & paste’ iliyotumika.

Diamond Snaps (65)

Video ya Diamond, Kidogo.

Siyo siri tena kwamba video hiyo iliyotoka wiki iliyopita ni kwamba imekuwa na mfanano mwingi wa mavazi na maudhui kutoka kwenye video tatu tofauti za wasanii wakubwa wa Marekani.

Taylor Swift (3)

Video ya Taylor, Shake It Off.

Kilichotokea ni kuwa Diamond amerudia kitu alichowahi kukifanya katika video ya Make Me Sing aliyoimba na AKA ambayo kwa kiwango cha juu alikopi video ya Got Money ya Lil Wayne. Kupitia gazeti hili niliandika juu ya mfanano huo, Februari 19, 2016.

Peter Okoye spika (5)

Video ya Diamond, Kidogo.

Nikianza na kipande cha mwishoni mwa video yake ya Kidogo, Diamond anaonekana akiwa na Simba pembeni ya kiti chake, kipande kama hicho kinapatikana kwenye moja ya kava za ‘series’ ya Empire inayomuonyesha Terrence Howard akiwa na Simba pembeni kwa mapozi na mavazi yaleyale.

487067248_640

Video ya Jasmine, That’s Me Right There.

Utetezi wa Diamond unaweza kuwa alichotaka ni kuonyesha yeye ni Simba kama anavyojiita lakini uhalisia ni kuwa alikopi na angeweza kubuni staili yake ambayo ingeweza kuleta mfanano wa jina la mnyama huyo.

Katika shairi la kwanza analoanza kuimba Paul Okoye, anaonekana katika meza ya chakula akiwa na mavazi, meza na viti vyeupe, ‘scene’ ambayo inafanana kila kitu na ile iliyopo katika video ya For The Road ya Tyga iliyowekwa mtandaoni Mei 24, 2013. Mfanano huo upo hadi katika ‘frame’ tupu zilizopo kwenye ukuta ndani ya video zote hizo.

Paul Okoye (1)

Video ya Diamond, Kidogo.

Kuna sehemu Tyga anaonekana akiwa na mbwa mwitu mweupe kwenye makochi meupe, kama kawa Diamond naye anapita mulemule, tofauti ni kuwa mhusika mmoja ni Mtanzania mwingine ni Mmarekani.

Kuna kipande Peter Okoye anaimba akiwa juu ya spika, mtazamo wa hapo unaendana kila kitu na video ya That’s Me Right There ya Jasmine V aliyomshirikisha Kendrick Lamar iliyotoka Agosti 22, 2014.

Copied Videos (11)

Video ya Tyga, For The Road.

Kama hiyo haitoshi, wadada wanaocheza (cheerleaders) kwenye Kidogo wamevaa nguo zinazofanana na wale wa kwenye Shake It Off ya Taylor Swift iliyotoka Agosti 18, 2014 kuanzia dizaini mpaka rangi za kijani na bluu za nguo hizo!

Diamond ni msanii anayevuka kutoka Afrika kuelekea Ulaya na Marekani, sasa kama anawaiga waziwazi kiasi hicho atakuwa na nguvu gani ya kuwaletea changamoto mpya kwenye ushindani wa kimataifa na hao anaowaiga kwa kila kitu!

Kufika levo za Tuzo za BET lazima wahusika watakuwa wanafuatilia kazi za Diamond, inapotokea wanaona vitu kama hivyo vinaweza kuchangia kumshusha kisanii.

Diamond mbwa (9)

Video ya Diamond, Kidogo.

Huu ndiyo mwanzo wa kuonekana ‘hana kitu’ na hata zile za awali alibahatisha au nazo ni za kukopi kazi ambazo hazijajulikana bado.

Kingine, uongozi wa Baba Tiffah unaweza kuwanyooshea kidole watengenezaji wa video hiyo, Godfather Productions kuwa wao ndiyo ‘master mind’ wa kila kitu katika hilo lakini je, ni wangapi wenye uelewa huo?

Tyga - For The Road (2)

Video ya Tyga, For The Road.

Nafikiri kuishiwa au kupoteza uwezo wa kufikiri ndiyo suala sahihi zaidi hapa, maana ilianza kwenye Make Me Sing na sasa tunayaona haya. Inajulikana kuwa hata msanii anaruhusiwa kupeleka mwongozo (script) wa anachokihitaji, sasa nani amefanya nini kati yao (Godfather na Diamond)?

Diamond eeeh! Kwa hapa ilipofika inatosha, ikiwezekana badili upepo au ongeza washauri na wajuzi wa mambo katika masuala ya video watakaoweza kung’amua mambo kabla ya mzigo kwenda hewani.

Tusidanganyane eti video ya Kidogo ikifika Amerika itaonekana mpya na kali wakati umeiba mawazo yao na kuyafanya katika kiwango kilekile au chini ya hapo, ukiiba au ukikopi unatakiwa ufanye kitu bora na uboreshe zaidi ya kule ulikochukua.

Leave A Reply