Mzee James Bukumbi enzi za uhai wake.
Padri akiongoza ibaada ya misa ya kumbukumbuku ya miaka minne tangu kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Global Publishers, Mzee James Bukumbi.
Mtoto wa Marehemu, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Publishers Marsha Bukumbi wakati wa misa hiyo.Ndugu jamaa na marafiki wakifuatilia ibaada ya misa.Padri akibariki makaburi ya wanafamilia waliotangulia mbele za haki.
Marsha Bukumbi akitoa neno.Watoto wa marehemu wa kiume wakiongozwa na Marsha kuweka shada kwenye kaburi la baba yao.
Mjukuu wa marehemu, Asteria akiweka shada kwenye kaburi la babu yake.
Watoto wa kike wa marehemu wakiweka shada kwenye kaburi la baba yao. Mtoto wa marehemu, Cosmas akiweka shada. Mafrateli wakiweka shada
Padri aliyeongoza ibaada ya misa akiweka shada.
KUMBUKUMBU ya miaka minne tangu kufariki kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Global Publishers & Gen. Enterprises Ltd, Mzee James Bukumbi imefanyika jana nyumbani kwa mareheu Kijiji cha Bupandwamhela, wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
Ndugu, jamaa na marafiki waliungana pamoja na na familia ya marehemu Mzee James Bukumbi katika ibada ya misa ya kumbukumbu iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Bupandwamhela.
James Bukumbi alizaliwa mwaka 1933 na kufariki dunia Agosti 25 mwaka 2012 jijini Dar es Salaam, mwili wake ulisafirishwa na kwenda kuzikwa nyumbani kwake kijijini Bupandwamhela.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN!
(PICHA: HILARY DAUDI/ GPL, BUPANDWAMHELA)