The House of Favourite Newspapers

Mwili wa Papa Wemba Wawasili DRC

0

PAPA WEMBA (1)

Kinshasa, Kongo

Mamia ya watu wamekusanyika leo nje ya Uwanja wa Ndege wa Kinshasa nchini Kongo wakisubiri mwili wa mwanamuziki aliyefariki Jumapili iliyopita, Papa Wemba kuwasili nchini humo.

PAPA WEMBA (6)Zoezi la kuuaga mwili wa marehemu Papa Wemba litafanyika wiki ijayo Jumatatu katika uwanja wa Kinshasa, DRC ambapo mashabiki wake pamoja na raia wote watatoa heshima zao za mwisho kwa mwanamuziki huyo.

PAPA WEMBA (4)Papa ambaye amefariki makiwa na umri wa miaka 66, ametajwa kuwa mmoja watu waliokuwa na ushawishi mkubwa Afrika ya Mashariki na kwamba ni miongoni mwa waanzilishi wa muziki wa kizazi kipya cha Soukous anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne ijayo baada ya kuagwa Jumatatu.

PAPA WEMBA (2)

Maafisa wa serikali na wanadiplomasia watahudhuria ibada ya kumkumbuka mwanamuziki huyo katika uwanja wa ndege kabla ya mwili huo kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.

Tamasha la bure la usiku kucha lilifanyika mjini Abidjan ambapo mwanamuziki huyo alianguka alipokuwa akiimba.

PAPA WEMBA (3)

Mwanahabari wa BBC Tamasin Ford anasema kuwa mashabiki wengi walivalia nguo nyeusi na kubeba mishumaa ili kutoa heshima kwa nguli huyo wa muziki.

PAPA WEMBA (5)

Mkewe Papa Wemba na wasaidizi wake pia walikuwepo.

Papa Wemba, who died aged 66, was considered one of Africa’s most influential musicians of his generation.

He pioneered modern Congolese soukous music, which spread through the continent.

Leave A Reply