Papa Misifa Atimuliwa Kaburu Records
Mmiliki wa kampuni ya Kaburu Records, Joseph Kaburu, akizungumza jambo na waandishi wa habari ( hawapo pichani).
ALIYEKUWA msimamizi wa kampuni ya Kaburu Records ambayo hurekodi muziki, upigaji picha na unamitindo, Papa Misifa, ametimuliwa katika kampuni hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii jana katika studio za kampuni hii zilizoko Sinza-Palestina jijini Dar es Salaam, mmiliki wa kampuni hiyo, Joseph Kaburu, amesema wamemtimu Misifa, kwa sababu hakuweza kuifikisha kampuni kwenye malengo waliyojiwekea.
“Sasa hivi tuna uongozi mpya kabisa kuanzia meneja na msemaji wa kampuni, Papa Misifa hatuko naye tena kwenye kampuni hii na wala hahusiki kabisa na chochote cha kampuni hii,” alisema Kaburu.