The House of Favourite Newspapers

Serikali Kuanzisha Tuzo za Mitandao ya Kijamii kwa Wanahabari

tbn-1

Mwandishi wa habari wa mtandao huu, Denis Mtima (kushoto) akikabidhiwa kadi ya kujiunga na mfuko wa hiari wa mwanachama wa PSPF na Waziri Nape Nnauye.

tbn-2

Nape akimkabidhi mwanadada mwandishi wa habari, kadi ya ATM ya NMB.

tbn-4

…Akisisitiza jambo fulani kwa wanahabari.

tbn-5

…Akizungumza jambo.

tbn-6

Mwakilishi wa wadhamini wa semina hiyo ambaye ni Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Vicky Bishubo, akizungumza jambo kwenye hafla hiyo.

tbn-7

Mkurugenzi wa mfuko wa hiari wa mwanachama wa PSPf, Adam Mayingu ambao nao walikuwa wadhamini wa semina hiyo, akizungumza jambo.

tbn-8

Vicky Bishubo akimkabidhi Nape zawadi iliyokuwa imeandaliwa kutoka NMB.

tbn-9

Taswira ilivyoonekana katika semina hiyo.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema serikali inatarajia kuanzisha Tuzo za Umahiri kwa waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii (blogs na website) kuanzia mwakani 2017.

Hayo ameyasema jana wakati akifunga semina kwa mtandao wa wamiliki wa mitandao ya kijamii na wanahabari nchini Tanzania maarufu kama Tanzania Bloggers Network (TBN).

Wakati huohuo alikabidhi kadi za ATM za NMB za kutolea fedha kwa wanahabari waliofungua akaunti zao za ‘Chap Chap Account’ na za kujiunga na mfuko wa hiari wa pensheni wa mwanachama (PSPF) jijini Dar es Salaam.

Semina hiyo ilikuwa ya siku mbili ambayo ililenga juu ya uendeshaji mitandao ya kijamii, namna ya kuzingatia maadili na namna ya kunufaika na mitandao hiyo kwa waendeshaji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Nape alisema serikali inaitambua mitandao ya kijamii (blogs na website) kuwa vyombo vya habari nchini kwani vina nguvu kubwa katika kupasha habari kwa jamii hata kuliko magazeti.

Alisema katika uchaguzi mkuu wa urais wa 2015 mitandao ya kijamii ndiyo iliyokuwa ikitumiwa kwani iliaminika kuwa ndiyo ingeweza kufikisha taarifa za matukio kwa urahisi na ilisaidia kwa kiasi kikubwa hata kupatikana kwa viongozi.

Na Denis Mtima/GPL

halotel-strip-1-1

Ilikupita hii? Magufuli Amnyoosha Shilole, Awa Mama Ntilie

Comments are closed.