The House of Favourite Newspapers

Shamsa Ford: Ku-date na staa ni kero sana!

0

SHAMSA (2)Wiki hii tunaye mwanadada anayefanya poa kwenye filamu Bongo, Shamsa Ford ambaye amepigwa maswali 1O na Mwandishi Wetu Gabriel Ng’osha. Unataka kujua kaulizwa nini akajibu vipi? Fuatilia hapa chini…

Ijumaa: Unaonekana uko kimya sana, mambo ya kufyatua filamu vipi?

Shamsa: Mambo yanaenda fresh, mipango inaendelea chini kwa chini na siku si nyingi vitu vizuri vitaonekana.

Ijumaa: Soko la filamu linaonekana kuyumba kiasi cha baadhi kugeukia kazi nyingine, unadhani sababu ni nini hasa?

Shamsa: Kikubwa kuangalia wapi tunakosea na naamini bado tunaweza kurudisha heshima ya filamu zetu na kuwa kama zamani.

Ijumaa: Tangu umeachana na Nay wa Mitego, uhusiano wako wa kimapenzi umekuwa wa siri sana, umeamua kuwa singo au una-date kimyakimya?

SHAMSA (1)Shamsa: Nipo na mtu ila siyo staa na wakati wa kumuweka wazi ukifika nitafanya hivyo.

Ijumaa: Au ndiyo yule Chid Mapenzi ambaye mara kwa mara mmekuwa mkionekana pamoja kimalovee?

Shamsa: Hapana, sina uhusiano na Chid Mapenzi, yule ni mshikaji wangu na tunashirikiana katika biashara.

Ijumaa: Umesema mpenzi wako wala siyo staa, kwa nini umeamua hivyo wakati uliwahi kusema kutoka na staa mwenzako kuna raha yake?

Shamsa: Nimegundua kuwa uki-date na staa ni kero, unafuatiliwa sana, kitu ambacho kinakosesha uhuru ndiyo maana nikaamua kubadilika.

Ijumaa: Kipi kilikuwa kinakukosesha amani ulipokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Nay?

Shamsa: Jinsi tulivyokuwa tunafuatiliwa maana ilikuwa hadi kero ndiyo maana hatukudumu.

Ijumaa: Kuna kipindi uliwahi kusema unavaa nguo za mitumba sana hata ‘makufuli’, huoni kwa staa kama wewe kuvaa nguo hizo ni kujishusha?

Shamsa: Noo, wala sioni tatizo maana nachagua zile zenye ubora kisha naziweka kwenye hali nzuri kabla ya kuzivaa.

Ijumaa: Unaizungumziaje serikali ya Magufuli?

Shamsa: Hakika mambo yanaenda vizuri, majipu yanatumbuliwa ila kwenye suala la mkwanja ndiyo kumebana ile mbaya.

Ijumaa: Unatofautisha vipi serikali ya sasa na ile iliyopita?

Shamsa: Tofauti ipo kwa kuwa uongozi ni wa watu wawili tofauti ila wote nawakubali, JK kafanya yake na Magufulia naye amekuja na kasi mpya.

Ijumaa: Kipi ambacho ungependa kuwaambia wasanii wenzako?

Shamsa: Kikubwa tupendane, tushirikiane, tuache majungu kwani kwa kufanya hivyo tutafika mbali na tasnia yetu itaheshimika.

 

Leave A Reply