The House of Favourite Newspapers

Steve Nyerere: Iyobo ametusitiri kwa Aunt

0

STEVE-NYERERESteve Mengere ‘Steve Nyerere’

Na Imelda Mtema

Staa wa filamu na vichekesho Bongo, Steve Mengere ‘Steve Nyerere’, amewavunja mbavu watu baada ya kusema kuwa anamshukuru sana Moses Iyobo kwa kukubali kuzaa na Aunt Ezekiel, kwani kwa kufanya hivyo amewasitiri wasanii wote wa Bongo Muvi.

AUNT NA IYOBOAunt ezekeiel na mpenzi wake, Mose Iyobo

Akizungumza wakati alipoalikwa kwenye bethidei ya mtoto wa mastaa hao iliyofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Serena jijini Dar, Steve alisema kuwa kitendo alichofanya Iyobo ni cha kishujaa sana kwani mpaka kumzalisha Aunt haikuwa kazi rahisi.

“Unajua watu wengi walishindwa lakini Iyobo ni kidume kabisa, tena katusitiria dada yetu na hatimaye sasa hivi ana mtoto. Ninachomsihi ni kuongeza mwingine fasta,” alisema Steve.

Leave A Reply