The House of Favourite Newspapers

Uwoya Aitwa Ikulu ya Kenya

0

Irene_Uwoya028Irene Pancras Uwoya.

IMELDA MTEMA, amani

DAR ES SALAAM: Zali! Kuna madai kwamba, Rais wa Kenya, Uhuru Jomo Kenyatta amempa mwaliko maalum staa mwenye mvuto katika sinema za Bongo, Irene Pancras Uwoya kuitembelea ikulu ya nchini hiyo, ikiwa ni msanii wa kwanza Bongo kupata fursa hiyo, Amani limedokezwa.

Kwa mujibu wa chanzo, awali rais huyo aliwahi kutolewa na jarida moja la nchini humo kwamba anazimikia sana kazi za filamu za staa huyo kutokana na filamu za Bongo Muvi.

Uhuru-Kenyatta-2.jpgRais wa Kenya, Uhuru Jomo Kenyatta

ATUMA WATU KUJA BONGO

Mpashaji wetu huyo alizidi kufunguka kuwa, Rais Uhuru aliwatuma wasaidizi wake kuja Bongo kumsaka staa huyo ambapo walipata maelekezo sahihi mpaka wakafika  nyumbani kwa wazazi wake,  Mbezi Beach jijini, Dar ambako walipata maelekezo sahihi ya kumpata Uwoya mwenyewe.

UJUMBE WAKUTANA USO KWA USO NA UWOYA

“Baada ya kuelekezwa jinsi ya kumpata Uwoya, walifunga safari mpaka Sinza Mori (Dar) nyumbani kwake anapoishi ambapo walifikisha ujumbe ambao walipewa na Rais Kenyatta. Irene alishtushwa  sana na ujumbe huo lakini baadhi ya watu wake wa karibu, wakiwemo nduguze walimtoa hofu.

“Walimwambia kwa rais kama Uhuru atakuwa anamuita kwa nia njema kabisa hivyo asiwe na wasiwasi maana yeye alijua labda kuna kitu alikosea sasa anakwenda kuwekwa kitimoto,” kilisema chanzo hicho.

UWOYA AKUBALI KUTINGA IKULU YA KENYA

Mpashaji wetu huyo alizidi kuanika kwamba, baada ya Uwoya kutolewa hofu  alikubali mwaliko huo na amepanga safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ajili ya kusikiliza wito huo.

AMANI LAMSAKA UWOYA

Baada ya kupata habari hiyo, gazeti hili lilimtafuta Uwoya, ambapo alikiri kupata mwaliko huo na kusema kuwa, kuna vitu anavikamilisha vikishakaa sawa atafunga safari ya kwenda huko kuitikia wito wa rais huyo.

“Ni kweli nimepata mwaliko huo na pia binafsi nimefurahi sana kwa kweli ila kuna vitu vyangu naviweka sawa baada ya wiki kama mbili hivi nitakwenda ili nikajue nimeitiwa nini,” alisema Uwoya.

KUMBUKUMBU

Hii si mara ya kwanza kwa Uwoya kuitwa ikulu ya nchi nyingine kwani mwaka 2011, Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza alimtumia ujumbe mwigizaji huyo akimtaka aende ikulu kwake kwa ajili ya mazungumzo ya kumtia moyo na sanaa yake, gazeti hilihili liliripoti.

Ilikuwa Julai 25, mwaka huo, Uwoya alisema Rais Nkurunzinza alimuita baada ya kusikia kuwa yupo nchini mwake na alivuta hisia za wengi kutokana na kazi zake za sinema.

Hata hivyo, katika mwaliko huo, Uwoya alishindwa kuonana na rais huyo kutokana na ratiba yake lakini aliombwa kutafuta siku kwenda kumtembelea rais huyo.

FILAMU ZATAJWA

Habari ambazo si rasmi zinadai kuwa, mwaliko wa Uwoya nchini Kenya unaweza kuchangiwa na kazi zake za sanaa ambapo, kwa sasa nchi za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, filamu za Bongo zinatazamwa na maelfu ya watu.

Leave A Reply