The House of Favourite Newspapers

Wanafunzi Wa St. Joseph’s Cathedral Walivyosherehekes Family Dar

0
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya St. Joseph’s Cathedral wakisali ibada fupi kabla ya kuanza kwa hafla fupi ijulikanayo kama ‘Family Day’.Wa kwanza kulia  Mkuu wa Shule ya St. Joseph Cathedral, Sista Theodora Faustine.
Wanafunzi wakiendelea na maombi kabla ya kuanza kwa Family Day.
Baadhi ya upande wa wasichana wa Shule ya St.Joseph’s walipokuwa wameketi wakiwa kwenye maombi mafupi kabla ya kuanza kwa hafla fupi ya Family Day.
Mkuu wa Shule ya St. Joseph Cathedral, Sista Theodora Faustine (katikati) akifuatilia kilichokuwa kikiendelea mbele kwenye hafla hiyo fupi ya wanafunzi ujilikanayo kama Family Day.
Baadhi ya wanafunzi wa St. Joseph’s wakionyesha vipaji vyao kwa kuimba nyimbo mbalimbali.
Mwanafunzi wa St. Joseph’s akionyesha kipaji chake kwa kuimba nyimbo mbalimbali.
w
Mwanafunzi akionyesha kipaji chake mbele ya wanafunzi wenzake.
Baadhi ya wanafunzi wakiigiza igizo kuonesha kipaji chao kama ishara ya hafla hiyo ya kusherehekea Family Day.
Mmoja wa wanafunzi akiimba nyimbo yake kwa hisia kali.
Wanafunzi wa St. Joseph’s wakiendelea na maigizo ya aina tofauti mbele ya wanafunzi wenzao kuashiria hafla hiyo fupi ya Family Day.
Wanafunzi wa St. Joseph’s wakifuatlia kwa makini igizo la wanafunzi wenzao lililokuwa likiendelea.
Baadhi ya wanafunzi wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikiendelea.
Mmoja wa wanafunzi wa St. Joseph akionyesha ujuzi wake kwa kupiga kinanda katika hafla hiyo.

 

Wanafunzi wa Shule ya Sekondaari ya St. Joseph’s Cathedral mapema leo wamesherehekea hafla fupi ijulikanayo kama Family Day ambayo imefanyika katika Hosteli zao zilizopo maeneo ya Don Bosco Osyter Bay jijin i Dar es Salaam.

 

Akizungumza na Global Tv Online mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo, Debora Sando alisema kuwa ni mkakati wao wa shule kila mwaka kukutana kwa pamoja kabla ya kufunga shule kuwa na siku maalum ya kufurahia ikiwa ni pamoja na kucheza michezo  kama vile kuimba nyimbo, kuigiza na mambo mbalimbali.

 

Wanafunzi hao kabla ya kuanza kwa hafla hiyo walianza kwa ibada maalum ambayo pia ilihusisha Mkuu wa Shule ya St. Joseph Cathedral, Sista Theodora Faustine ambaye alikuwa sambamba na wanafunzi hao kuhakikisha mambo yote yanaenda sawa.

 

 

Leave A Reply