The House of Favourite Newspapers

Wazee Wanaobebwa na Penalti Bara

0

MSIMU mpya wa Ligi Kuu Bara unaendelea   kusonga mbele timu zikiwa zimecheza  mpaka mechi 13 ingawa bado kuna baadhi ya timu zipo nyuma na zina viporo.

 

Lakini pamoja na hayo yote, bado ufundi unazidi kuonekana kwenye ligi hiyo huku ushindani ukiendelea kushika kasi ya hali ya juu kwa timu hata kwa mchezaji mmojammoja na wengi wakionekana kuwa wapya.

 

Msimu huu mpaka sasa kwenye Ligi Kuu Bara kinara wa ufungaji amefunga mabao nane ambaye ni Meddie Kagere wa Simba lakini inaonekana kuwa penalti zimembeba kufikia hapo alipo. Msimu huu umekuwa na ushindani mkubwa sana.

 

Tumeona wachezaji wengi wakipambania timu zao na kufunga mabao mengi ya penalti hadi sasa.

 

MEDDIE KAGERE- SIMBA

Huyu licha ya kuwa kinara wa mabao kwenye ligi kwa sasa, lakini katika mabao ambayo amefunga, mawili ni ya penalti, Alianza mbele ya Kagera Sugar wakati Simba

ya JKT  ambao walitoa sare 2-2 alifunga kwa penalti na sasa Azam ina pointi 19 katika mechi tisa walizocheza.

AWESU AWESU- KAGERA

Ameifungia Kagera mabao manne mpaka sasa kwenye ligi, katika mabao hayo moja alifunga kwa penalti na ilikuwa dhidi ya KMC pale Uwanja wa Uhuru na kuisaidia timu yake kushinda 2-1.

 

PETER MAPUNDA – MBEYA

Huyu timu yake inapumulia mashine kwani imekuwa na matokeo mabovu msimu huu ikiwa ikishinda mabao 3-0 pia alifunga dhidi ya Mbeya City na kusaidia Simba kushinda mabao 4-0.

SAID DILUNGA -RUVU

Kwenye Uwanja wa Sokoine, Prisons iliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting ambapo bao lao pekee hilo la kufutia machozi lilifungwa na kiungo fundi Said Dilunga dakika ya 25 kwa penalti.

 

AGGREY MORIS- AZAM

Mpaka sasa amecheza mechi mbili baada ya kurejea kutoka kwenye majeraha ambayo alipata kipindi cha michuano ya Afcon. Amecheza dhidi ya Alliance Schools na JKT Tanzania, lakini kwenye mchezo dhidi nafasi ya 19.

 

Katika Uwanja wa Sokoine kwenye mchezo kati yao na Mwadui FC, straika huyo alifunga bao moja kwa penalti na kushuhudia kikosi chake kikilala kwa mabao 2-1 lakini pia alifunga penalti nyingine dhidi ya Mbao FC.

 

Wengine ambao walifunga kwa penalti ni; David Kameta wa Lipuli dhidi ya Prisons na mechi iliisha sare kwa mabao 2-2. Rajabu Zahir wa Ruvu dhidi ya JKT Tanzania na JKT kushinda mabao 2-1. David Molinga wa Yanga ana mabao manne kwenye ligi hadi sasa hana bao hata moja la penalti.

Leave A Reply