Yvonne Nelson ahamishia mapenzi kwa Bismark
Staa wa filamu Ghana na Nigeria, Yvonne Nelson akiwa na mpenzi wake mpya Bismark Nii Odoi ‘Bismark The Joke.’
STAA wa filamu anayebamba Ghana na Nigeria, Yvonne Nelson baada ya kutemana na mpenzi wake, John Dumelo ameamua kuhamishia mapenzi kwa mchekeshaji maarufu Ghana, Bismark Nii Odoi ‘Bismark The Joke.’
Kupitia kurasa za Instagram za Bismark na Yvonne zimeanika wazi picha zao mbalimbali wakiwa katika mapozi ya kimahaba.
Bismark katika pozi.
Pia katika mahojiano na TV ya News One ya Ghana, Bismark alikiri kwa kusema kuwa Yvonne ni mke wake mtarajiwa.
Wawili hao walianza kuwa karibu tangu walipokutana katika filamu ya If Tomorrow Never Comes.
Comments are closed.