MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli leo alikuwa, katika Uwanja wa Bombardier Singida Mjini ambako alifanya mkutano wa kampeni, ikiwa ni miongoni mwa vituo vya kampeni zake alizofanya leo, Septemba 1, 2020
Baadhi ya kauli alizozitoa kwenye kampeni zake hizo ni:
“Mimi siwezi kusema mkinichagua kodi nitafuta, utaendeshaje nchi, siwezi kufuta kodi. Hata Ulaya wanalipa tena wana sheria kali kweli, tutaendelea kulipa kodi inayowezekana, ndiyo maana Wamachinga tumewawekea kodi ya Sh 20,000 kwa mwaka.
“Kuna watu wanasema tutafanya hivi, tutafanya vile, hizo ni ndoto, kuongoza nchi si mchezo ni kazi kubwa, huwezi kusema mimi mkinichagua kila kitu nitawaletea na wala huwezi sema mimi mkinichagua hamtolipa kodi, utaendeshaje nchi bila kodi?
“Nchi hii ilikuwa shamba la bibi, kila mahali tulikuwa tunaibiwa. Tena hata Watanzania wenzetu walikuwa wanatetea wezi. CCM imeweka umeme kwa vijiji 9,570 ndani ya miaka mitano na haiwezi kushindwa vichache vilivyobakia.