Dubai yamnyoosha Vera
Vera Sidika katika Pozi
Vera Sidika na vazi la Baibui Dubai
Over Ze Weekend: Gazeti la Ijumaa Wikienda, Toleo la Jumatatu, Jan. 16, 2017
MWANAMITINDO Vera Sidika amejikuta ananyooka mwenyewe baada ya kutua Jiji la Dubai na kushindwa kutupia vinguo vyake (nusu utupu) na kuvaa vazi la Baibui.
Tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo, katika picha mbalimbali zilizovuja zinamuonesha Vera akiwa kwenye vazi la baibui kitendo ambacho si cha kawaida kwake ambapo wapo mashabiki waliomsifu na wengine kumnanga kuwa jiji hilo limemyoosha. Vera amezoeleka kama mtu wa kujiachia nusu utupu bila kujali mazingira.