The House of Favourite Newspapers

Hawa Ndiyo Walibebwa na Kolabo Wakatusua Bongo

darasaKILA msanii huwa na njia zake za kupita kabla ya kuja kutusua na kuteka mashabiki. Kuna wale ambao wametoka wakiwa wenyewe kwenye nyimbo zao na wale wengine am­bao wametumia migongo ya wenzao kuweza kute­sa.

Suala la msanii mmoja kumshiriki­sha mwenzake ‘kolabo’, ni jambo la kawaida lakini kuna wasanii ambao wali­tumia nafasi hizo kuweza kutambulika katika ulimwengu wa sanaa na hivi sasa wamekuwa nyota ambao wana­tikisa vilivyo.

Ingawa kuna listi ndefu ya wasanii ambao wamefani­kiwa kutoka kwa kutumia kuwashirik­isha wasanii wenzao la­kini hii hapa ni orodha ya miongoni mwa wasanii ambao kolabo na wasa­nii wenzao ziliwabeba na sasa wanatamba.

darassaDARASSA

Nani asiyemjua msa­nii huyu ambaye ngoma yake ya Muziki imem­fanya kuwa maarufu kwa rika zote kuanzia watoto hadi watu wazima?

Lakini mafanikio aliyo­nayo leo msanii huyu anayejulikana kama Shar­iff Thabeet, yalitokana na kolabo yake aliyofanya na msanii mwenzake, Ber­nard Paul ‘Ben Pol’ katika Wimbo wa Sikati Tamaa ambao ndio ul­iomtambuli­sha katika tasnia ya muziki wa Bongo.

Wakati Darassa anau­toa wim­bo huo hakuwa na umaarufu wa kihivyo lakini Ben Pol tayari al­ishaliteka soko kutoka­na na mikwaju yake ya Ni­kikupata na Samboira na baada ya hapo wameen­delea kuwa na ukaribu wa pamoja na hata sasa wote wanatamba na Wimbo wa Muziki ambao wameshirikiana tena.

moyo-sukuma-damu-3DITTO

Msanii ambaye ame­uambia moyo wake usu­kume damu na uachane na kujipa kazi za vitu vingine, naye anaingia kwenye makala haya kwa sababu aliju­likana kwenye ulim­wengu wa sanaa kutokana na kolabo ambayo ndiyo imemfanya afike hapa alipo.

Kwa wale wa­naomsikia sasa Ditto, kila kitu chake kwenye muziki wake kili­badilika baada ya kufanya ngoma n a Suleiman Msin­di ‘Afande Sele’ katika mkwaju wa zamani wa Darubini Kali ambao ulim­pa mafanikio ma kubwa, hasa kujulikana kwa jamii.

malaika77MALAIKA

Ni miongoni mwa wa­dada ambao wanafanya vizuri katika chati ya muz­iki wa Bongo kutokana na baadhi ya nyimbo zake kama Mwan­tumu , Sare Sare, Zogo na Raruararua lakini umaaru­fu wake ulikuja baa­da ya kupata shavu la ku­piga kolabo na msanii Chegge katika Wimbo wa Uswazi Take Away.

Tangu ashirikishwe katika wimbo huo, Malaika hajafanya makosa ya kupotea kwani ame­kuwa akitoa nyimbo ambazo zinaende­lea kumpa nafasi ya kutamba hapa nchini.

steve-rnbSTEVE RNB

Ni miongoni mwa wasanii ambao wana­ ufanya Muziki wa RnB kuendelea kuwa ka­tika chati hapa nchini. Naye alijulikana baada ya kufanya kolabo.

Wapenda muziki wa hapa nchini wal­ianza kumuelewa za­idi baada ya kushirik­ishwa kwenye Wimbo wa Ta­basamu wa Mr Blue ambao aliufanyia kazi kwelik­weli kwenye kiitikio na baada ya ngoma hiyo mambo yakam­u endea vyema.

shettaSHET­TA

Nur­din Bilal ndiyo jina lililo kwenye hati zake za kusafiria lakini kwa wale wap­enda muziki wanamtambua kama Shetta ambaye amewa­hi kutamba na ngoma kali kama Namjua, Nidan­ganye, Kerewa, Mdananda na ny­ingine.

Lakini yote hayo yalikuja baada ya ngoma yake ya Nimechokwa am­bayo alimpa shavu Mbongo Fleva mwen­zake, Abednego Dam­ian ‘Belle 9’ ambaye kwa kipindi hicho alikuwa anatamba mi­taani na pini yake ya Sumu ya Penzi. Baada ya kolabo hiyo, Shetta ameendelea kuwika vilivyo hadi kufani­kiwa kupiga kolabo na wasanii wakubwa Afrika kama Mnigeria, KCEE katika Ngoma ya Shikorobo.

ommy-dimpozOMMY DIMPOZ

Staa wa nyimbo ya Achia Body am­baye naye umaarufu wake kwenye muziki wa Kizazi Kipya ume­kuja baada ya kupitia mgongo wa kolabo.

Wakati anatoka Ommy Dimpoz am­baye hati yake ya kusafiria ina jina la Omari Faraji Nyembo, alifanya ushirikiano na Ally Saleh Kiba ‘King Kiba’ kwenye Ngoma ya Nai Nai ambayo ili­mpa jina na umaarufu mkubwa kutokana na kumshirikisha nyota ambaye alishajiten­genezea mizizi ka­tika muziki huu.

BILNAS BILLNAS CHAFU POZI GREGORY ALLSTARTZ DAR MULTITECH ZONEBILL NASS

Hana muda mrefu kwenye ‘game’ ya muziki wa Kizazi Kipya lakini ngo­ma zake za Chafu Pozi, Raha na Ligi Ndo­go zimemfanya awe maarufu.

Lakini umaarufu huo umetokana na kolabo ambazo amezifanya na wasa­nii nguli, Naaziz wa Kenya kwenye Raha kablaya ku­hamia kwa Top in Dar (T.I.D) am­baye aliwahi kuwa kion­gozi wake katika Radar Enter­tain­ment am­bapo kuto­kana na kolabo hizo, anaende­lea kutikisa vilivyo. Ali­shirikiana na T.I.D kwenye Ligi Ndo­go

Comments are closed.