The House of Favourite Newspapers
gunners X

Sister Fay Sipendezi Nikivaa Nguo za kike

Sister Fay akiwa Sebuleni mwanaye

Na IMELDA MTEMA| RISASI JUMAMOSI| MPAKA HOME

MAMBO vipi mpenzi msomaji wangu, kama kawaida kila wiki ndani ya safu hii maridhawa ya Mpaka Home ni kuwatembelea mastaa mbalimbali majumbani mwao na kufanya nao mahojiano. Leo tunaye mwanamuziki wa kitambo kidogo, Faiza Omary ‘ Sister Fay’ lakini hivi karibuni ameibuka upya baada ya kutoa wimbo wake uitwao Kaja Mwenyewe.

Mwanamuziki huyu ambaye pia ni muigizaji anaishi maeneo ya Kinondoni Mkwajuni na mtoto wake wa kiume pamoja na ndugu zake wengine. Amezungumza mambo mengi kuhusiana na maisha yake ya kila siku nje na kazi yake, ungana nami ili uweze kuyafahamu.

Fey akipanga vitabu

Maisha yake ya kawaida yakoje?

Fey akipaweka mayai katika friji

“Maisha yangu hayana tofauti na ya watu wengine, naishi maisha ya kawaida kama unavyoniona hapa hakuna kilichobadilika kwangu kabla sijawa staa na nilivyo sasa, sina tofauti na watu wengine. Ameolewa? Nimeolewa lakini kwa bahati mbaya sana mume wangu haishi hapa yuko nchini Uingereza na kwa kweli ananipa sapoti kubwa katika ishu zangu za sanaa, namshukuru sana kwa hilo.

Fey akiwa jikono

Anawezaje kuishi mbali na mumewe, kuhusu michepuko kumsumbua?

Fey akiwa Jikoni

“Unajua hayo mambo kama mwanamke anajifanya hawezi kuishi muda mrefu bila kuwa na mumewe karibu ni kujiendekeza tu, kikubwa kama hauna tamaa na umejenga uaminifu kwa umpendaye haina shida na michepuko haina nafasi kwenye maisha yangu.

Kwa nini anapendelea kuvaa nguo za kiume?

“Mimi najiona sina umbo zuri la kuvaa nguo za kike sipendezi na nikagundua nikivaa za kiume angalau zinaficha umbo langu ndiyo maana napenda ila nikienda sehemu ambazo zinahitajika kuvaa mavazi kama hayo, navaa bila shida.Vipi ni mtaalamu katika mapishi?

“Katika hilo napenda kujipongeza ni mtaalamu na ninajua kuliteka jiko kama mwanamke niliyefundwa nikafundika najiamini kwa hilo na mume wangu anapenda sana mapishi yangu na ninafikiri kitu ambacho anakimisi zaidi akiwa mbali nami ni mapishi yangu.

Alishawahi kulala sebuleni?

Wakiwa chumbani

“Mara nyingi sana tena kipindi hiki nilichokuwa narekodi wimbo wangu ni balaa, nikirudi tu nikisema nijipumzishe sebuleni napitiwa na usingizi, nikishtuka ni asubuhi basi nanyata mpaka chumbani

ili wadogo zangu wasinione kuhofia watanicheka.

Kitu gani kilimuumiza maishani?

“Nilipowapoteza wazazi wangu niliumia sana na bado kinaendelea kuniumiza mpaka leo. Anaishije na majirani zake? “Uzuri wewe umekuja umeweza kushuhudia mwenyewe kwa macho yako ninavyoishi nao vizuri na kama mtu hajawahi kuniona kwenye runinga wala kusikia wimbo wangu anaweza kujua mimi ni mtu wa kawaida.

Fey akifanya usafi

Nini matarajio yake ya baadaye? “Napenda kufika mbali niwe na maendeleo mengine zaidi ya hapa, natamani kuwa na nyumba kwa sababu bado napanga. Kwa nini alikuwa akisema Magali ni baba yake mzazi wakati siyo?

“Hiyo ilikuwa kupaishana tu majina lakini kulikuwa hakuna ukweli wowote wala hatuna undugu.”                 

Fey akikunja nguo
Fey na Mwanaye

 

Wakiwa chumbani

Comments are closed.