The House of Favourite Newspapers

Mr Shinda Nyumba Ajimwaga Mitaa ya Keko

Mr Shinda Nyumba akigawa vipeperushi kwa wasomaji katika mitaa ya keko

ILE bahati nasibu ya Shinda Nyumba inayoendelea kwa sasa chini ya Kampuni la Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Championi, Ijumaa, Amani na Risasi inazidi kusonga mbele ambapo watu mbalimbali wanaendelea kujitokeza na kujaza kuponi kwa wingi ili kutengeneza nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali kila mwezi zikiwemo pikipiki na simu za kisasa na hatimaye kujishindia nyumba katika droo kubwa itakayochezeshwa  baadaye mwaka huu.

…Akimpa maelekezo msomaji wa magazeti ya Global Publishers, Samila Ramadhani, mkazi wa Keko jinsi ya kujaza kuponi.

Huku bahati nasibu hiyo ikiendelea kuwa gumzo kutokana na msisimko iliyonayo, leo Mr Shinda Nyumba anayesepa na kijiji kila kona anakopita alikuwa mitaa ya Keko jijini Dar alikowatembelea wasomaji na wananchi kwa jumla kwa mara nyingine.

…Akimjazia kuponi Samila Ramadhani baada ya kununua Gazeti la Ijumaa Wikenda.

Mbali na kumshangaa Mr Shinda Nyumba, wakazi wa maeneo hayo walijitokeza kwa wingi huku wakionyesha dhahiri kupania kujishindia nyumba pamoja na zawadi mbalimbali.

…Akimjazia kuponi Amani Chilingo, msomaji wa magazeti ya Global Publishers.

“Hii nyumba lazima niipate, nimeshiriki hii bahati nasibu toka mwakani, kiukweli nimepania sana kwa mwaka huu lazima nikate kuponi niwezavyo ili  kushinda nyumba,”  Vincent George mfanyabiashara katika mitaa hiyo.

Dereva wa Global Publishers, Kefa Masaga, akimpa maelekezo Sophia Samson, mkazi wa Temeke wakati akijaza kuponi.
Kefa akiwa na msomaji wa magazeti ya Global baada ya kujaza kuponi.
Shinda Nyumba akiwagawia vipeperushi wasomaji wa magazeti ya Global wanaofanyia shughuli zao maeneo ya Keko.
Mr Shinda Nyumba akiwapa maelekezo wasomaji wa magazeti ya Global ya jinsi ya kujaza kuponi.
Mr Shinda Nyumba akimshuhudia Juma Mwaipopo, anayefanyia biashara maeneo ya Keko wakati akijaza kuponi
Msomaji wa magazeti ya Global, Rehema Hassan, mkazi wa Pugu-Kipogo akichana sehemu ya kuponi kwenye gazeti baada ya kununua gazeti na kujaza kuponi.

Kwa upande wa mwanamama Rehema Hassan alisema kuwa bahati ya kushinda nyumba ni ya kina mama na amepania kwa mwaka huu  ataibuka na nyumba hiyo huku akisisitiza ataendelea kukata kuponi bila kukoma.

“Mimi nimeamua mpaka kieleweke, kila siku nakata kuponi moja tu, najua shilingi mia tano ninayowekeza kila siku ni lazima itarudi mwishoni mwa bahati nasibu hii,” alisema Rehema.

Boniphace Ngumije/GPL

Comments are closed.