The House of Favourite Newspapers

Vita ya Warner Bros vs 20 Century vs Marvel

Batman.

INAWEZEKANA mpaka leo hii bado Bongo Muvi wanajifikiria namna ya kutoka na kutengeneza pesa ya nguvu, wanaoandaa filamu hawajui ni kwa namna gani wanaweza kutoka na kuweka ladha tofauti katika filamu zao.

Superman.

Wakati sisi tunajifikiria hivyo, wenzetu hasa Hollywood wamepiga hatua na sasa hivi kuna vita kali inaendelea katika watengenezaji wa filamu nchini Marekani, ni vita kubwa ambayo inawafanya kutengeneza pesa kila siku iendayo kwa Mungu.

Kila mwaka kampuni za muvi, Warner Bros, Marvel na 20th Century Fox zinakuja na mawazo mapya, ni kwa namna gani wanaweza kutengeneza fedha kwa kuwaandaa waigizaji wa ajabu (comic) ambao sasa hivi wamekuwa wakipendwa na kuwafanya watu kuingiza fedha kwa kiasi kikubwa.

20th Century Fox.

MAMBO YAPO HIVI

Walianza Warner Bros. Hii ni kampuni inayomilikiwa na wanaume wanne waliotoka kwenye familia ya Warner. Baada ya kuingia kwenye filamu wakawaandaa wahusika wao kama Superman, Batman, Joker, Green Lantern na wengineo miaka ya 1970.

Waliikamata dunia, walitengeneza sana fedha kiasi kwamba leo unaposema Superman au Batman kila mtu anawafahamu. Baada ya miaka mingi na kuona kwamba Marvel wanakuja kasi, wakaongeza wahusika wengine kama Wonder Woman na wale wote wanaopatikana kwenye filamu ya Suicide Squad ikiwa na Will Smith.

Avatar.

Wakati Warner Bros wakiendelea, kwa upande wa Marvel, walichokifanya ni kuwaweka wahusika wao. Wakamtengeneza Spiderman, kweli akawa maarufu, akapendwa na kuwapa fedha nyingi, baada ya hapo wakawatengeneza Ironman, Hulk, Captain America, Black Panther na mwaka huu wamemtengeneza mwingine aitwaye Dr. Strange.

WAWAKUSANYA PAMOJA

Wakati utata wa wahusika wa kampuni ipi wapo bomba zaidi ya wengine, walichokifanya Marvel ni kuwachukua wahusika wake wengi na kuwaweka pamoja kwa kutengeneza muvi iitwayo Avengers ambayo ilikuwa na wahusika kama Ironman, Hulk, Thor, Black Widow baadaye wakamuweka BlackPanther, Antman, Spiderman ambao waliingia kwenye muvi ya Captain America: Civil War.

Kwa ujumla Avengers imeingiza dola bilioni 1.405 (zaidi ya shilingi trilioni mbili). Mbali na hayo, pia wakaanzisha filamu za Deadpool, X Men ambayo zimekusanya mastaa wengi wakiwemo Magneto, Professor X na wengine wengi na kwa filamu hizo pia wakafanikiwa kuingiza kiasi kikubwa cha fedha.

Warner Bros wakaona kama wamefunikwa, na wao walichokifanya ni kutengeneza muvi ambayo ilikuwa na waigizaji wao kwa pamoja, wakatengeneza ya Superman vs Batman iliyotoka mwaka huu, humo wakamuweka Wonder Woman na filamu hii ikaingiza dola bilioni 872 (zaidi ya trilioni moja) na inaendelea kuingizampaka leo.

20th CENTURY FOX WAZEE WA KIMYAKIMYA

Wakati hayo yote yakiendelea, 20th Century Fox hawana hofu,wamekaa pembeni na wanaangalia jinsi mchezo unavyochezwa na wenzao. Wanajiamini kwa sababu wana mtu anaitwa James Cameron ambaye ndiye aliyetengeneza muvi za Terminator zilizochezwa na Schwarzenegger, Titanic na Avatar.

KWA NINI 20th CENTURY WANAMUAMINI CAMERON?

Huyu jamaa anaweza kuitwa ‘genius’ kutokana na filamu zake zinavyobamba. Kwanza unatakiwa kujua kuwa filamu yake ya Titanic ndiyo iliyokuwa ikiongoza kwa kuingiza fedhanyingi duniani kuliko filamu zote kabla ya rekodi hiyo kuvunjwa na Avatar mwaka 2009.

Mpaka sasa filamu hiyo (Titanic) imeingiza dola bilioni 2.187 (zaidi ya trilioni 4.5). Baada ya hapo, kuonyesha k w a m b a alikuwa si mtu wa mchezomchezo, akaandaa filamu nyingine iitwayo Avatar ambayo ilivunja rekodi na kuipitia Titanic, mpaka sasa ndiyo imekuwa filamu iliyoingiza kiasi kikubwa cha fedha, dola bilioni 2.788 (zaidi ya trilioni 6).

Hawa washikaji wanawaangalia wenzao (Marvel na Warner Bros) wanavyopambana kila mwaka kwa kutengeneza filamu zao kwa kuwaweka mastaa wengi mno ila tangu 20th Century Fox watengeneze filamu yenye watu wa ajabu ya Avatar mwaka 2009, mwaka huu wanakuja na Avatar 2 ambayo vipande vyake (trailer) vitaanza kuonyeshwa mwaka huu.

Wanachojua ni kwamba filamu yao itakuja kuzikimbiza zote za Avengers na Superman vs Batman kwa kuwa tu wana mtu sahihi. Je, unahisi Avatar 2 itaifunika ile ya kwanza na kuuza zaidi? Unahisi hawa Marvel na Warner Bros wataweza kuwafunika 20th Century? Yetu macho.

 

Comments are closed.