The House of Favourite Newspapers

Mtifuano wa Shirikisho la Azam Wafikia Patamu

0
Wawakilishi wa timu zilizoingia nusu fainali ya Shirikisho la Azam.
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa, Idd Moshi Shaaban, akichanganya majina ya timu hizo kabla ya kuitoa moja baada ya nyingine.
Wanahabari na wadau wakifutilia droo hiyo kwa makini.
Baada ya zoezi hilo kumalizika wadau wakiongea hili na lile.

Mtifuano wa Kombe la Shirikisho la Azam leo umefikia patamu baada timu zitakazomenyana katika nusu fainali kujulikana baada ya droo iliyofanyika ofisi za uzalishaji za Azam Media zilizopo Tabata jijini Dar.

Katika droo hiyo Simba itakuwa mwenyeji ambapo itapambana na Azam FC Aprili 29 mwaka huu jijini Dar ambapo Yanga itakwenda Mwanza kupambana na Mbao FC watakaouwa wenyeji wa mchezo huo.

Baada ya droo hiyo wawakilishi wa timu hizo kila mmoja alijinasibu kuonyesha umahiri wake kwenye mchezo huo.

Simba iliwakilishwa na Mjumbe wa Kamati yake ya Utendaji, Said Tuli, Yanga iliwakilishwa na meneja wake, Afidh Saleh, Mbao FC iliwakilishwa na mratibu wa timu hiyo, Masalida Zefania, ambapo Azam iliwakilishwa na Meneja wa timu hiyo, Philip Alando.

(PICHA/ HABARI: RICHARD BUKOS / GPL)       

Leave A Reply