WAKATI Droo Ndogo ya Tano ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba Awamu ya Pili ikiendelea kubamba kila kona ya nchi, wasomaji wa Gazeti Amani ambalo ni moja kati ya magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya Global Publishers, wameonekana kupagawishwa baada ya kunaswa maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar wakilinunua kwa kasi, lengo likiwa ni kujishindia zawadi mbalimbali.
Mr. Shinda Nyumba aliyekuwa kwenye mishemishe za kuitangaza bahati nasibu hiyo ndiye aliyewabamba wasomaji hao Alhamisi iliyopita maeneo ya Mbagala wakinunua gazeti hilo na kujaza kuponi zilizokuwa ndani ili waibuke washindi.
Wakati hayo yakiendelea, taarifa nyingine nzuri ni kwamba zawadi kibao zikiwemo pikipiki, simu, Dinner Set, TV na nyinginezo zinatarajiwa kutolewa kwenye droo ndogo ya tano inayotarajiwa kuchezeshwa Julai 20, mwaka huu.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Global Publishers, wachapishaji wa magazeti ya Championi, Ijumaa, Amani, Uwazi, Risasi na Ijumaa Wikienda, Yohana Mkanda amesema mahali ambapo shughuli hiyo itafanyika itafahamika siku chache zijazo.
“Ninachoweza kuthibitisha ni kuwa droo hii ya tano itafanyika Julai 20, kuna vitu vidogo tunavifanyia kazi ili tuweke wazi mahali ambapo shughuli yetu itafanyika,” alisema Mkanda.
Kabla ya droo hiyo ya tano, tayari Global Publishers imeshafanya droo ndogo nne ambazo zilifanyika katika maeneo ya Mbagala Dar Live, Manzese Bakhresa na CCM Mwinjuma Mwananyamala (mara mbili).
Katika droo hizo zote, washindi wamekuwa wakipewa zawadi mbalimbali ambazo zimebadili maisha yao, zikiwemo pikipiki, televisheni, simu za kisasa za mikononi, vyombo vya nyumbani na ving’amuzi kutoka Kampuni ya Ving’amuzi vya Ting.
“Kwenye magazeti yetu yote, katika kurasa za pili zipo kuponi zenye maelekezo ya namna ya kufanya, ukishamaliza kujaza, unaweza kuzituma kwetu kupitia kwa mawakala wetu waliopo nchi nzima au wale wa Dar wanaweza kuja ofi sini kwetu, Bamaga Mwenge na kuziacha kwenye ndoo ya kukusanyia kuponi,” alisema Mkanda wakati akiwaelekeza wasomaji namna ya kujaza kuponi hizo.
Bahati Nasibu hii imedhaminiwa na Kampuni ya Tecno Mobile, King’amuzi cha Ting, British School na Kilimanjaro Institute of Technology.