UHAKIKI WA RIWAYA: WATOTO WA MAMA N’TILIE
UHAKIKI WA RIWAYA: WATOTO WA MAMA N’TILIE
MWANDISHI: EMMANUEL MBOGO
WACHAPISHAJI: HEKO PUBLISHERS
MWAKA: 2002
MHAKIKI: DAUD MAKOBA
UTANGULIZI
Watoto wa Maman’tilie ni kitabu kinachogusa jamii katika nyanja zote. Tunaona watoto wakifukuzwa shule kwa kukosa ada. Umasikini uliokithiri ni chanzo cha maovu ya kutisha: Ujambazi, biashara ya madawa ya kulevya, rushwa na mabaya kedekede chanzo chake ni ufukara. Riwaya hii inazidishwa utamu na mlevi mtiifu – Mzee Lomolomo, ambaye hana habari na familia yake, yupo katika vilabu akinywa chang’aa!
MAUDHUI
Dhamira
- Watoto wa mitaani na hatima yao. Watoto wanapoteza mwelekeo wa maisha pale wanapofukuzwa shule. Zita, Peter, Musa, Kurwa na Doto wanajihusisha na vitendo viovu vikiwemo vya uuzaji wa madawa ya kulevya.
- Wizi na ujambazi. Watoto wadogo, Kulwa, Doto na Dan wanajiingiza katika ujambazi. Wanakwenda kuvamia katika duka la Mhindi, huko, Doto na Dan wanauawa kwa kupigwa risasi na mlinzi Simango… BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI