UHAKIKI WA RIWAYA: TAKADINI
MWANDISHI: BEN J. HANSON
WACHAPISHAJI: MATHEWS BOOKSTORE AND STATIONARIES
MWAKA: 2004
MHAKIKI: DAUD MAKOBA
UTANGULIZI JUU YA UHAKIKI WA RIWAYA: TAKADINI
TAKADINI ni riwaya inayopaza sauti kuwatetea watu wenye ulemavu. Katika jamii za Kiafrika walemavu hawakupewa kipaumbele. Wengi waliuawa na waliopona walitengwa!
Katika riwaya hii, mwanamke shujaa, Sekai anaukataa ujinga wa jamii yake dhidi ya walemavu. Anajitolea kufa na kupona kutetea uhai wa mwanaye mwenye ulemavu wa ngozi – TAKADINI.
MAUDHUI
DHAMIRA
- Ukombozi wa kiutamaduni. Jamii inawatenga watu wenye ulemavu. Mzee Makwati na washikilia mila za kale wengine wanadhamiria kumuua Takadani kwa sababu alizaliwa akiwa mlemavu wa ngozi. Sekai anatoroka na mwanaye ili kumuepusha na balaa hilo… SOMA ZAIDI