The House of Favourite Newspapers

Niyonzima: Nikiwafunga Yanga Nitashangilia

0
Kiungo wa Simba, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima.

KIUNGO wa Simba, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima, ameweka wazi kuwa endapo timu yake hiyo itaibuka na ushindi kwenye mchezo wao dhidi ya Yanga, basi atashangilia.

 

Niyonzima ambaye ali­jiunga na Simba mwanzoni mwa msimu huu akitokea Yanga, amebainisha hilo ikiwa ni siku chache kabla timu hizo hazijakutana.

Oktoba 28, mwaka huu ni siku ambayo Yanga na Simba zina­tarajiwa kupambana kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar.

 

Akizungumza na Global TV Online, Niyonzima alisema mchezo baina ya Simba na Yan­ga siku zote huwa ni mgumu, lakini ameonyesha dhamira yake ya kushangilia bila ya kuhofia chochote ikitokea wao wamepata ushindi na kama yeye akifunga.

 

“Hakuna asiyejua ugumu wa mechi baina ya Simba na Yanga, katika mechi zinazokuwa na kukamiana kwingi ni hizo, hivyo nitafurahi kama tukipata pointi tatu dhidi yao au nikifunga nitashangilia japokuwa itakuwa kiungwana siyo kwa nyodo na dharau.

 

“Zaidi naomba siku tukikutana tupate pointi tatu tu maana ndiyo kitu cha muhimu kwetu, ili tuweze kufikia mafanikio yetu ya kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu, ni lazima tupate pointi tukicheza na Yanga, Azam na Singida United.

 

“Hizi ndizo timu kubwa kwa sasa na ndiyo ambazo naona zina upinzani mkubwa kwetu, hivyo ili upate ubingwa kwa sasa ni muhimu pia uhakik­ishe unapata pointi katika timu hizo,” alisema Niyonzima. Kushuhudia mahojiano kamili, tembelea akaunti ya Global TV Online kwenye mtandao wa YouTube.

Stori: Musa Mateja

Leave A Reply