Kajala Kuasili Mtoto Wa Kulea
STAA kiwango kunako filamu Bongo, Kajala Masanja amesema kuwa yuko mbioni kuasili mtoto kwenye kituo kimoja cha kulelea watoto yatima jijini Dar.
Akizungumza na Star Mix, Kajala alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona mtoto wake wa kwanza, Paula ameshakuwa msichana mkubwa hivyo hawezi tena kubeba mimba kwa hivi sasa.
“Nilikuwa na wazo hilo muda mrefu sana lakini sasa naona ndio wakati umefika wa kufanya hivyo kwa kuwa naona wazi siwezi kuzaa tena, bora nimchukue mtoto kwenye kituo nimlee mwenyewe mpaka akue.”