The House of Favourite Newspapers

Timu Tatu Zamuibukia Ronaldo Madrid

Cristiano Ronaldo.

STAA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo inasemekena amepokea ofa kutoka klabu tatu za Ulaya. Real Madrid ilipokea ofa tatu, wiki iliyopita na kumpelekea Cristiano Ronaldo.

 

Hata hivyo, haijawekwa wazi mara moja majina ya klabu zilizokuwa zimetoa ofa hizo. Taarifa zaidi zinasema kuwa klabu moja maarufu ilikuwa tayari kuandaa ofa ya kufa mtu ili kumnasa mchezaji huyo bora wa dunia.

 

Katika siku za karibuni kumekuwa na maneno kuwa Ronaldo ameuomba uongozi wa Real Madrid umruhusu kuondoka katika klabu hiyo.

Uongozi wa Real Madrid, hata hivyo, umegoma kumruhusu Ronaldo ahame na badala yake wanamwandalia mkataba mpya.

Comments are closed.