Museveni Akubaliana Na Trump ‘Kuwananga’ Waafrika
RAIS Yoweri Museveni wa Uganda amesema anampenda Rais wa Marekani, Donald Trump, kwa kusema ukweli baada ya kuzishambulia baadhi ya nchi duniani zikiwemo za Afrika ambazo alisema ni “chafu”.
“Anawaambia Waafrika ukweli,” alisema Museveni baada ya kauli hiyo ya Trump ambayo ilishutumiwa sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Afrika. MusevenI alisema hajui kama Trump alinukuliwa vibaya, hata hivyo hilo si tatizo kwani rais huyo husema ukweli, na mtu hawezi kuwa imara iwapo ni mnyonge.
Viongozi kadhaa wa Afrika wakiwemo marais Nana Akufo-Addo wa Ghana na Hage Geingob wa Namibia, walishutumu lugha hiyo.
Trump alitumia maneno hayo akiwa ikulu ya Marekani, Januari 12, mwaka huu ambapo yalishutumiwa na baadhiya watu kuwa ni ya “kibaguzi, ya kushitua na ya aibu”.
WALUSANGA NDAKI/MITANDAO/MASHIRIKA
Comments are closed.