The House of Favourite Newspapers

Salamba.. Mabao Matano, Anawaza Kumfikia Okwi

Emmanuel Okwi

NI mmoja kati ya wachezaji am­bao wameku­ja na kuwe­za kuinusuru Lipuli FC ambayo ni wazi licha ya kupam­bana lakini jahazi lake lilikuwa na dalili ya kuzama kutokana na safu ya usham­buliaji kuoneka­na kuwa butu.

 

Hii ni kutokana na Lipuli kupata pigo la kuondokewa na beki wake mahiri, Mghana, Asante Kwasi ambaye alikuwa msaada katika upachikaji mabao ambapo mpaka anak­wenda Simba alikuwa ame­funga mabao matano na sasa Lipuli im­efunga jumla ya mabao 16 kwenye mechi 22 za Ligi Kuu Bara.

Adam Paul Salamba (kushoto) akipitia mkataba kabla ya kuusaini

Baada ya k u o n d o k a , timu hiyo ilitu­mia dakika 540 ambazo sawa na mechi tano kuweza kufun­ga tena bao a m ­bapo waliibu­ka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Stand United.

 

Huyu si mwingine bali ni msham­buliaji Adam Salamba am­baye anaoneka­na kama ndiye anayeibeba Lipuli kwa sasa kuto­kana na uwezo wake wa kupachi­ka mabao tangu asajiliwe kipindi cha dirisha dogo.

S a l a m b a a m e f a n i k i w a kucheza mechi nane tangu asa­jiliwe kipindi cha dirisha dogo na amefunga mabao matano kwenye michezo hizo.

 

Haya ni se­hemu ya maho­jiano kati yake na Championi Ijumaa ambapo anaelezea masuala yake ya soka.

ULIANZIA WAPI KUCHEZA SOKA?

“Soka la ushindani nilianza kucheza mwaka 2014 nikiwa timu ya Ligi Daraja la Pili inayofahamika kwa jina la Bulyanhuru ya Shinyanga ambayo ili­kuwa ikidhaminiwa na Kampuni ya Acacia.

“Lakini nikiwa hapo niliitwa timu ya Maboresho ya Vijana U-23 na Ko­cha Mart Nooij na Salum Mayanga.

“Baada ya hapo nilibahatika kusajiliwa na Geita Gold, ulikuwa msimu wa mwaka 2015/16, nili­cheza pale lakini mechi moja pekee tukaanza kusumbuana kwenye suala la malipo na timu ilikuwa ipo Ligi Daraja la Kwanza, hivyo nikaach­ana nao.

 

“Nikatimkia Zanzibar kwenye kikosi cha Polisi Zanzibar, hapo nili­cheza nusu msimu nikaamua kuon­doka, nikaenda kufanya majaribio Mtibwa Sugar, kwa bahati mbaya walimu wa pale hawakunielewa, ikabidi niondoke tu.“Nikarudi Shin­yanga kwenye timu yangu ya Buly­anhuru wakati huo nikawa nasubiri dirisha kubwa lifunguliwe.

 

ILIKUWAJE UKATUA STAND UNITED?

“Nilikwenda Stand United kufanya majaribio kipindi cha ‘pre-season’ bahati nzuri nilikutana na yule ko­cha Mfaransa, Patrick Liewig, aliku­bali uwezo wangu, nikawa nimesa­jiliwa hapo.

 

“Msimu uliopita ndiyo nilianza kuichezea Stand United, bahati nzuri mechi ya kwanza tulicheza na Azam FC pale Kambarage niki­tokea benchi nilifanikiwa kufunga bao moja ambalo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo, nilifurahi sana sababu ilikuwa mara ya kwanza kucheza ligi kuu na nimefanikiwa kuifunga timu kubwa kama Azam.

 

“Lakini katika mzunguko wa kwanza nikiwa na Mfaransa siku­weza kupata sana nafasi ya kucheza zaidi nilikuja kupata kwenye raundi ya pili baada ya Kocha Hemed Mo­rocco kuanza kuinoa Stand na mpa­ka msimu unaisha nilifunga mabao manne pekee.

 

TUKIO GANI LILIWAHI KUKUUMI­ZA KATIKA SOKA?

“Na k umb u k a baada ya kuihama Stand na kutua Lipuli, tulipoche­za

kulipwa wakasahau kabisa fadhila na kuweza kunifanyia vile jambo ambalo si zuri.

 

TOFAUTI KATI YA STAND NA LIPULI NI IPI?

“Tofauti ipo kubwa, nilipokuwa Stand nilipewa majukumu mengi ndiyo maana haikuwa rahisi sana kuweza kufunga mabao sababu straika nilikuwa mwenyewe.

“Upande wa Lipuli nimepewa ju­kumu la kufunga tu ambapo nime­kuwa nikisaidiana na wenzangu, ndiyo maana inakuwa rahisi kuweza kufunga.

 

CHANGAMOTO IPI UMEPATA MSIMU HUU?

“ Kwa n z a kitendo cha mimi ku­tua Lipuli FC ulikuwa ni mtihani m k u b w a sana kwan­gu hasa ki­mazingira, awali nili­pata shida kutokana na baridi, h i v y o n i k awa naugua kifua mara kwa mara na ilini­chukua muda mrefu kuzoea mazin­gira na kuanza kufanya vizuri.

 

UNADHANI UNAWEZA KUWA MFUNGAJI BORA MSIMU HUU?

“Licha ya ushindani kuwepo kwenye ligi na mimi nikiwa nime­funga mabao matano sijakata tam­aa bado ninaamini kuwa naweza kumpindua Emmanuel Okwi pale alipo sasa na nikawa mfungaji bora sababu lolote linaweza kutokea.

“Bado tuna mechi nane mkono­ni, huwezi jua mechi ijayo naweza kupiga ‘hat trick’ au nikafunga hata mabao manne, hilo linawezekana na nikiweka juhudi naweza kuwa mfungaji bora msimu huu.

 

VIPI USHINDI KWENYE LIGI?

“Ushindani umekuwa mkubwa kwa sasa katika ligi jambo ambalo limekuwa mtihani kwa timu nyingi sababu ukiteleza mechi moja basi unashuka na ukishinda tu unapan­da hasa kipindi hiki cha lala salama.

 

MALENGO YAKO NI YAPI?

“Kwanza kuhakikisha nafanya vyema msimu huu kwa kutimiza malengo yangu na ya klabu kama ambavyo tumejiwekea kuhakiki­sha tunamaliza tukiwa katika tano bora, hivyo tunapambana kutoka pale kwenye nafasi ile ya saba mpaka kuingia nafasi tatu za juu.

 

KWA NINI UNAPENDA KU­VAA JEZI NAMBA 10?

“Hii kwangu ni kama namba yenye bahati kwangu ndiyo maana nilivaa nilipokuwa Stand na sasa hapa naendelea kuitumia.

 

BEKI GANI ANAYEKUSUM­BUA UWANJANI?

“Beki ambaye ananipa mawazo hasa ninapokaribia kukutana naye ni Aggrey Moris wa Azam FC amekuwa akinitesa sana kuliko mabeki wengine hata (Kelvin) Yondani mwenye hamfikii Moris, yuko vizuri siyo rahisi kukabiliana naye na kum­shinda.

 

MASHABIKI WATEGEMEE NINI KUTOKA KWAKO?

“Wategemee mazuri tu lakini kikubwa ni kuendelea kutupa sa­poti na wasichoke naamini msimu huu tutamaliza vizuri licha ya ush­indani kuwa mkubwa,” anasema Salamba.

Comments are closed.