The House of Favourite Newspapers

Sportpesa Super Cup Imetuvua Nguo, Tujipange

NIANZE kutoa kongole kwa Mbwana Samatta na Ally Salehe Kiba ‘King Kiba’ kwa kile ambacho waliki­fanya mwishoni mwa wiki iliyo­pita kwa kutumia vipawa vyao kwa ajili ya kuchangia maen­deleo ya elimu hapa nchini.

 

Kwangu ni wazo zuri ambalo li­natakiwa kuungwa mkono pale litakapokuja kufanyika kwa mara ya pili kwani tumeona ushiriki wa watu kwa kiasi fulani hauku­wa mkubwa kama ilivyotarajiwa.

 

Lakini pia nitoe rai kwa mastaa wengine kuiga na kufanya kama vile au zaidi na walivyofanya Kiba na Samatta kwa kuchangia kidogo kwa kile ambacho wanakipata kuto­ka kwa jamii ambayo inawasapoti.

Baada ya hapo sasa nageukia kweye kile ambacho ndicho kimeni­fanya nishike kalamu na kuandika makala haya. Wikiendi iliyopita pale Kenya kulikuwa na fainali ya michua­no ya SportPesa Super Cup ambapo Simba ilipambana na Gor Mahia.

 

Baada ya dakika 90, Simba wali­jikuta wakipewa kipigo cha ma­bao 2-0 na kombe hilo kutua tena kwa Gor Mahia ambao mara ya kwanza walilichukua hapa jijini Dar mwaka jana, hivyo wamejipatia na­fasi ya kwenda kucheza mechi ya kirafiki na Everton nchini England.

 

Kikubwa siyo kwamba tume­poteza nafasi ya kwenda kuche­za na Everton katika Uwan­ja wa Goodson Park, bali ni mazingira ya ushiriki kwa timu zetu.

 

Ukiangalia mwanzo mpaka mwisho kwa jinsi ya timu zetu zilivyoshiriki ni kama hazikuwa na maandalizi mazuri kwani mwan­zoni tu Yanga walivurumishwa ka­tika michuano hii kwa kufungwa na Kakamega Home Boys. Baa­daye JKU ya Zanzibar nayo ika­tolewa kwa kufungwa na Gor Mahia.

Wawakilishi wetu wengine, Singi­da United na Simba nao hawakuwa na matokeo ya kuridhisha licha ya kwamba ndiyo wameshika na­fasi ya tatu na pili. Katika mechi zote tatu walizocheza, Singida United hawakufanikiwa kupata ushindi ndani ya dakika 90 zaidi ya kubebwa na penalti hadi wa­nakamata nafasi hiyo ya tatu.

Ukija kwa Simba, wao nao licha ya kwamba ndiyo walicheza fainali na Gor Mahia, lakini katika daki­ka 270 ambazo ni sawa na mechi tatu walizocheza, hawakufanikiwa hata kufunga bao moja ndani ya muda huo. Walikuwa wanasonga mbele kwa mikwaju ya penalti.

 

Jambo hilo linonyesha kwamba jinsi ya timu zetu zilivyo pamoja na mfumo mzi­ma wa ligi yetu inavyokwenda.

Inashangaza sana kuona bingwa wa nchi anakwenda kwenye mi­chuano halafu anamaliza mechi tatu bila hata kupata bao.

Sidhani kama kwa mwendo huu tunaweza kuwa na matu­maini ya kuona timu zetu ziki­fanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika na Ligi ya Mabingwa Afrika.

 

Nadhani kwa kupitia michuano hiyo ya SportPesa iwe fundisho kubwa kwetu kuona kwamba tuna­takiwa kubadilisha juu ya mwenen­do wetu na kuboresha baadhi ya mambo kuona tunatoka kwenye tope ambalo tumekwama sasa na kwenda mbele zaidi kama tu­nataka kuona timu zetu zinapata mafanikio kwenye ngazi za klabu hasa kwa upande wa kimataifa.

 

Tunatakiwa kuangalia matokeo waliyoyapata Simba, Yanga, JKU na Singida United kwenye michuano hiyo, kisha tuyafanyie kazi kweli kwa ajili ya kuzijenga timu zetu ili hata iki­tokea kwa wakati mwingine michua­no hii inatokea basi tufanye vizuri.

Comments are closed.