The House of Favourite Newspapers

RUBY BAND &THE MAFIK BAND, BENDI BONGO FLEVA TISHIO

The Mafik Band.

ILIPOIBUKA Yamoto Band mashabiki wengi waliona mapinduzi ya Muziki wa Bongo Fleva kupitia bendi yamefika. Ni kweli Yamoto Band ikiwa na vichwa vinne, Maromboso, Becka Flavour, Enock Bella na Aslay ilisumbua katika muziki huo huku ikifanikiwa kutoa vibao vikali sambamba na kupata shoo kibao ndani na nje ya nchi.

Sio hivyo tu, Yamoto Band ndiyo bendi ya kwanza kutokea kwenye Muziki wa Bongo Fleva ikiwa imeweka historia kibao ya ‘kuzurura’ kwenye majukwaa mengi ya siasa katika kampeni pamoja na sherehe mbalimbali za kitaifa.

Ukiachana na hilo, zipo bendi zilizoi­buka lakini zikaam­bulia za uso kama vile Skylight Band na nyingine nyingi. Kwa sasa zimeibuka bendi mbili za Muziki wa Bongo Fleva zinazokimbiza kwa kasi am­bazo ni Ruby Band pamoja na The Mafik.

Over Ze Weekend limefanikiwa kuzipata bendi hizo na kuzi­fanyia mahojiano moja kwa moja, hizi hapa zisikie;

RUBY BAND

Over Ze Weekend: Mashabiki wangependa kujua bendi yenu ina wasanii wangapi?

Ruby Band: Bendi ina wasanii wa kuim­ba wawili ambao ni C Minor pamoja na Kwela TZ. Ukiungan­isha kuanzia wapiga drums, madansa na watu wengine wa vo­cal jumla tupo 12.

Over Ze Week­end: Tumeona bendi nyingi zinakuja kwa kasi na kupotea, vipi kwa upande wenu?

Ruby Band: Kuna kitu ambacho tume­kiunda sisi kama sisi cha ushirikiano kwa kila mmoja. Tulipoanza waimbaji tulikuwa wanne lakini kutokana na tabia mbovu kundini wawili walifukuzwa na sasa waim­baji tumebaki wawili ambao tunajielewa.

Over Ze Weekend: Nani anayewa­tungia na mpaka sasa mna ngoma ngapi?

Ruby Band: Kwa sasa tuna Ngoma ya Kuntu tuliofanya kwa C9 Kanjenje. Ngoma nyingi tulizofanya zamani tukiwa wanne hatuwezi kuzitumia. Kuhusu ku­tunga huwa tunatunga wenyewe wakati mwingine tukishirikiana na uongozi.

Over Ze Weekend: Mlishawahi kufiki­ria kuwaongeza wasanii wa kike kwenye bendi yenu?

Ruby Band: Hilo limekaa kiungozi zaidi, kwa sasa tunafikiria tusonge tukiwa wawili kwanza.

Over Ze Weekend: Mnapiga ‘live band’ au ndio wale wa kuiga CD kwa nyuma?

Ruby Band: Tuna uwezo mkubwa wa kuchanganya, tunapiga kuanzia akapela, live band mpaka playback inategemea shoo tunaopiga.

Over Ze Weekend: Asanteni sana.

THE MAFIK

 

Over Ze Weekend: Nani aliwapa wazo la kuita bendi yenu The Mafik?

The Mafik: Wazo lilitoka kwa uongozi ambao ulikuwa unasimamia Club ya Cube ambayo kila Jumapili walikuwa wanaalika wasanii kwa ajili ya kupafomu ‘Extreme Sunday’ kuna baadhi ya wasanii ambao wa­likuwa tayari wapo na wanafanyakazi hapo kama vile Enock, Mbalamwezi na wadada wengine wawili kwa hiyo hao walikuwa hapo ‘Official’ kama wanamuziki wa bendi ya hapo.

Over Ze Weekend: Nini maana ya The Mafik?

The Mafik: Mafik ni neno la Kikongo linalimaanisha Bahati kwa hiyo The Mafik naweza nikasema tumebahatika na ili uwe na bahati ni lazima ubarikiwe kwa hiyo sisi tumebarikiwa.

Over Ze Weekend: Mna menejimenti?

The Mafik: Yeah, tunayo.

Over Ze Weekend: Mnasimamiwa na nani?

The Mafik: Tupo chini ya King Empire.

Over Ze Weekend: Mna nyimbo ngapi?

The Mafik: Zipo nyingi tu ambazo hazijatoka kama 20 ila ambazo tumeziachia tayari ni tatu, ambayo ni Passenger, Carola na Sheba.

Over Ze Weekend: Ni mafanikio yapi ambayo mmeyapata?

The Mafik: Makubwa sana kwa sababu Passenger ni wimbo ambao umewe­za kupokelewa kwa ukubwa sana ukizingatia ni wimbo wetu wa kwanza lakini umepokelewa kwa ukubwa sana na siwezi nikasema ni mafanikio gani ila mafanikio ni mengi hadi kualikwa kwenye matamasha makubwa kama South Africa kwenda kufanya performance.

Over Ze Weekend: Nani huwa anawa­tungia nyimbo?

The Mafik: Tunaandika wenyewe na wote ni waandishi wazuri lakini hatuzuii mtu yeyote mwenye idea ya wimbo kutubariki tuimbe tunawakaribisha sana.

Over Ze Weekend: Majina yenu wote kwa usahihi?

The Mafik: Mimi naitwa Hamadi Has­san lakini jina la muziki ni Hamadai, kuna Mbalamwezi anaitwa Abdallah Yusuph na Rhino anaitwa Salehe Kheri.

Over Ze Weekend: Asanteni sana.

The Mafik: Karibu!

 

 Story:SHAMUMA AWADHI

Comments are closed.