The House of Favourite Newspapers
gunners X

Richard Tanganyika Akabidhiwa Pikipiki ya ‘Tusua Maisha na Global’

Mshindi wa pikipiki katika shindano la Tusua Maisha na Global, Richard Tanganyik,  akiongea na wanahabari baada ya kukabidhiwa funguo za pikipiki yake leo katika ofisi za Global Group zilizooo Sinza-Mori jijini Dar es Salaam.
Ofisa Usambazaji, Keffa Massaga (kushoto) akimkabidhi funguo  za pikipiki, Richard Tanganyika.
Tanganyika akiwa na zawadi yake.
Washindi wakiwa na zawadi zao.
Washindi na wafanyakazi wa Global Group.

MSHINDI wa pikipiki katika Shindano la Tusua Maisha na Global, Richard Tanganyika, amekabidhiwa zawadi yake pamoja na washindi wengine  katika ofisi za Global Group, zilizoko Sinza-Mori jijini Dar es Salaam.

Washindi wengine waliokabidhiwa zawadi zao ni Shaaban Kamoye aliyejishindia dinner set, Nasoro Juma aliyejishindia headphones za kisasa, za Beats by Dre na Novart Magere aliyejishindia jezi, ambaye amewakilishwa na ndugu yake, Hassan Mathias.

 

Kushinda ni rahisi, nunua gazeti lolote la #GlobalPublishers la #Uwazi#Amani#Ijumaa#IjumaaWikienda#RisasiMchanganyiko#RisasiJumamosi#Championi#SpotiXtra kisha fuata maelekezo ukurasa wa pili.

(PICHA: RICHARD BUKOS | GPL)

Comments are closed.