The House of Favourite Newspapers

Ronaldo Agawa 53m Ya Zawadi

Mchezaji wa Juventus, Cristiano Ronaldo.

MUDA mfupi baada ya kuanza maisha ya kuwa mchezaji wa Juventus, Cristiano Ronaldo ameonyesha kuwa yeye ni mtu wa watu.

 

Ronaldo, 33, alikuwa nchini Italia siku kadhaa zilizopita ili kukamilisha dili lake la kusajiliwa na Juventus, inaelezwa kuwa akiwa hotelini alipofi kia alifurahishwa na huduma aliyopatiwa kutoka kwa watoa huduma na ndipo akaaamua kuwapa fedha wagawane.

 

Akiwa hotelini hapo na baadhi ya memba wa familia yake, kabla ya kuondoka aliwaita wale wote waliokuwa wakiwahudumia na kuwapa pauni 17,850 (Sh milioni 53) kama zawadi ya huduma nzuri na kuwaambia wagawane.

Comments are closed.