The House of Favourite Newspapers

JAJI MKUU WA TANZANIA ATEMBELEA OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella, Mhe. Jaji Mkuu alipata wasaa wa kutoa pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na wananchi wote waliopatwa na maafa ya kivuko cha MV Nyerere yaliyotokea Septemba, 20, 2018 katika wilaya ya Ukerewe.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella nakala ya kijitabu cha Mpango Mkakati wa miaka mitano (5) wa Mahakama ya Tanzania, pindi Mhe. Jaji Mkuu alipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huyo, wa pili kushoto ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza, Mhe. Sam Rumanyika.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella (wa nne kushoto), Mhe. Jaji Mkuu aliyetembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza mwishoni mwa wiki iliyopita aliambatana na Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Mhe. Jaji Sam Rumanyika (wa tatu kulia) na baadhi ya Maafisa wa Mahakama mkoani Mwanza.

 

 

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma  amefanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella, nakupata wasaa wa kutoa pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na wananchi wote waliopatwa na maafa ya kivuko cha MV Nyerere yaliyotokea Septemba, 20, 2018 katika wilaya ya Ukerewe.

 

Aidha; Mhe. Jaji Mkuu alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ushirikiano katika ya ofisi yake na Mahakama mkoani humo.

 

 

(Picha kwa hisani ya Ibrahimu Mohamedi, Mahakama Kuu Mwanza)

 

 

Comments are closed.