USIKU wa kuamkia leo wapenzi wa burudani waliofurika ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live huko Mbagala-Zakhem, walipata uhondo bab’kubwa kwenye onyesho la Usiku wa Mwambao lililokutanisha miamba ya muziki na kusindikizwa na burudani zingine kama vile muziki wa Singeli kutoka kwa Sholo Mwamba na Kibao Kata kutoka kwa mkali wa kuchagiza almaarufu kwa jina la Kivurunde.
Burudani hiyo iliwafanya mashabiki wapagawe na kujimwaya uwanjani mwanzo-mwisho huku zikichezwa staili mbalimbali zilizokuwa zikinogesha usiku huo.
Makundi yaliyotoa burudani kwenye onyesho hilo ni First Class linaloongozwa na Athuman Sudi a.k.a Amigo; Ogopa Kopa linaloongozwa na Malkia wa Mipasho, Khadija Khopa; Yah TMK linaloongozwa na Omary Tego na dada yake Maua Tego, na vikundi vingine vya burudani.
PICHA: RICHARD BUKOS | GPL
Comments are closed.